STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, September 24, 2012

Simba yazidi kupaa Ligi Kuu Tanzania Bara

Amri Kiemba wa Simba ajijaribu kumtoka beki wa Ruvu katika pambano lao la jana
 
MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, Simba, wameendeleza wimbi la ushindi wa asilimia 100, baada ya kuibuika na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Ruvu Shooting, pambano lililochezwa leo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Simba ilipata bao la kuongoza dakika ya 30, likiwekwa nyavuni na nyota wa kimataifa wa Zambia, Sunzu kwa kichwa maridadi akimalizia krosi iliyopigwa baada ya kazi nzuri ya kuwachambua mabeki iliyofanya na Said Nassor ‘Cholo’ aliyepanda kusaidia mashambulizi.

Dakika 38, Kiemba akawachachafya wachezaji wa Ruvu, kabla ya krosi yake kukosa mmaliziaji na kuishia mikononi mwa Benjamin Haule.

Simba iliendelea kushambulia ambapo katika dakika ya 44, beki Mau Bofu wa Ruvu alimwangusha Sunzu ndani ya 18 na mwamuzi Swai kuamuru ipigwe penati. Akuffor akabeba jukumu la kupiga tuta hilo, ambalo mlinda mlango Haule alipangua na kuwa kona tasa.

Hadi mapumziko, Simba ilitoka ikiongoza kwa bao hilo, huku mashabiki waliohudhuria mechi hiyo wakishuhudia maamuzi tata ya mwamuzi Swai, aliyeonekana dhahiri kutowajali vibendera wake Samwel Mpenzu na Godfrey Kihwili wote wa Arusha pindi wanapoashiria madhambi.

Kipindi cha pili kilianza kwa Ruvu kushambulia lango la Wekundu na kama si umakini mdogo miongoni mwa washambuliaji wake Paul Ndauka, Hussein Said na Hassan Dilunga aliyekuwa akipenya kirahisi safu ya ulinzi, wangeweza kupata mabao.

Sunzu akafanya shambuliazi kali dakika ya 55 lililotokana na jitihada binafsi akiwalima chenga mabeki, kabla ya Ruvu nao kurudi langoni mwa Simba na Dilunga (Hassani) nusura aipatie bao timu yake, kabla ya mawasiliano madogo na Abdulrahman Mussa kumgharimu.

Ruvu ikapata bao la kusawazisha mnamo dakika ya 78, lililowekwa nyavuni na mtokea benchi Seif Rashid, akitumia makosa ya beki Juma Nyoso wa Simba, aliyeshindwa kuondoa hatari langoni akiwa peke yake na kuukanyaga mpira huo na kuteleza, ambapo Seif aliunasa na kumchambua Juma Kaseja.

Daniel Akuffor akimtoka beki wa Ruvu Shooting


Wakati wengi wakimiani matokeo ya pambano hilo yangebaki kuwa ni sare ya bao 1-1, mtokea benchi wa Simba, Christopher Edward aliyeingia kuchukua nafasi ya Akuffor, akaipatia timu yake bao la pili dakika ya 87 kwa shuti na kuamsha mamia ya mashabiki wake jukwaani.

No comments:

Post a Comment