STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, September 24, 2012

Yanga kupokwa ushindi dhidi ya JKT Ruvu?

Kikosi cha timu ya Yanga

LICHA ya kuchekelea ushindi wa mabao 4-1 iliyopata dhidi ya JKT Ruvu, mabingwa wa Kombe la Kagame, Yanga huenda wakapokwa ushindi wao huo iliyopata juzi kwenye uwanja wa Taifa, jijini Dar iwapo itabainika wakikiuka kanuni za ligi juu ya idadi ya wachezaji wa kigeni kucheza mechi moja.
Yanga katika mechi yao na JKT iliwachezesha wachezaji wake wote watano wa kigeni, kitu kinachoelezwa ni kinyume na kanuni inayoruhusu klabu kuwatumia wachezaji wasiozidi watatu kucheza mechi moja ya ligi.
Katika pambano hilo la juzi Yanga iliwachezesha mapro wake wote akiwamo kipa Yew Berko, beki Mbuyu Twite, kiungo Haruna Niyonzima, mshambuliaji Didier Kavumbagu na winga Hamis Kiiza.
Micharazo, imedokezwa kwamba uongozi wa Simba tayari unajiandaa kuwasilisha barua ya kupinga kitendo kilichofanywa na watani zao za kuwatumia wachezaji wake hao wa kigeni katika mechi moja, ingawa tunaendelea kufuatilia kuona kama Yanga ilikiuka kanuni ya ligi kuhusu wachezaji au la...
Kama itakuwa imekiuka kuna uwezekano Yanga wakajikuta wakipokwa ushindi huo na kuzidi kuwasononesha baada ya kutoka kwenye machungu ya kushindwa kufurukuta katika mechi zao za awali ambapo ililazimishwa suluhu na Prisons Mbeya kabla ya kulala mabao 3-0 kwa Mtibwa Sugar.


No comments:

Post a Comment