STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, September 5, 2012

Mzee Yusuf aanzisha kampuni kusambaza kazi ili kudhibiti wezi

NYOTA wa muziki wa taarab nchini, Mzee Yusuf 'Mfalme' amefungua kampuni yake binafsi ya usambazaji wa kazi zake na wasanii wengine iitwayo MY Collection. Akizungumza na MICHARAZO, mkurugenzi huyo wa kundi la Jahazi Modern Taaran alisema ameamua kufungua kampuni hiyo ili kusaidia kuthibiti uchakachuaji na wizi wa kazi zake ambao umekuwa ukimkomesha mapato mengi. Alisema kampuni hiyo ambayo imeshafungua duka la kuuzia cd na dvd katika mitaa ya Likoma na Mhonda itakuwa ikihusika na usambazaji na uuzaji wa kazi za Jahazi Modern na zile za wasanii wengine iwapo watapenda kufanya hivyo kwake. "Katika kukabiliana na vitendo vya wizi wa kazi zangu, nimeamua kufungua kampuni ya usambazaji na uuzaji wa cd na dvd ambayo itahusika na kazi zote za Jahazi Modern, ila kama kutakuwa na watakaotaka kuwasaidia kusambaza kazi zao sitakuwa na noma," alisema. Naye Meneja Masoko wa kampuni hiyo, Mussa Msuba duka walillofungua litakuwa likihusika na kuuza kazi za taarab kwa jumla na rejereja ili kuwarahisishia mashabiki wa muziki huo eneo la kupata burudani hiyo. "Hili ni duka la awali tu, pnago ni kufungua karibu kila kona ya nchi kuwarahisishia mashabiki mahali pa kupata burudani za taarab kwa matumizi yao ya majumbani na ya kibiashara kwa ujumla na hasa kazi za Jahazi ambao wanatarajia kutoa albamu mpya ya tisa," alisema Msuba. Uamuzi wa Mzee Yusuf kufungua kampuni na duka hilo, imekuja mwezi mmoja baada ya kunasa baadhi ya albamu zake zilizochakachuliwa walipoendesha msako wakishirikiana na wadau wengine wa sanaa wakiwemo Shirikisho la Filamu Tanzania, TAFF na Bongo Movie.

No comments:

Post a Comment