STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, October 13, 2012

Mashali, Sebyala wapima uzito kuvaana kesho Friends Cornerupimwa uzito kesho


BONDIA Thomas Mashali wa Tanzania na Mganda Medi Sebyala wamepima uzito leo kwenye ukumbi uliopo Manzese jijini Dar es Salaam tayari kwa ajili ya pambano lao la ubingwa wa Afrika Mashariiki na Kati litakaofanyika Jumapili kwenye ukumbi wa Friend's Corner, Manzese jijini Dar es Salaam.
Mabondia hao walipimwa uzito na afya hizo asubuhi ya leo tayari kwa pambano hilo lililoandaliwa na mratibu Regina Gwae chini ya TPBO.
Mbali na mabondia hao wengine waliopimwa leo ni  Abdul Awilo atakayepanda ulingoni kuchuana na Shedrack Juma, Selemani shaaban atakayechapana na Hamis Mohamed,  Jonas Segu atakayemkabili Ibrahim Class  na  Charles Mashali atakayevaana na Teacher Aaron.
Regina alisema maandalizi yote yamekamilika ikiwamo waamuzi wenye sifa za kuchezesha mapambano ya kimataifa anbao tayari wameshapatikana na mgeni rasmi katika pambano hilo atakuwa Kamanda wa  Mkoa wa Kipolisi Kinondoni, Charles Kenyela ambaye anatarajiwa kuambatana na wageni wengine maalum akiwamo Mbunge wa Jimbo la Kinondoni, Mhe. Idd Azzan.
---

No comments:

Post a Comment