STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, December 4, 2012

Bwana Misosi avunja ukimya na mpya

Bwana Misosi katika pozi

STAA wa kitambo wa muziki wa Bongofleva, ambaye kwa sasa amejitosa kwenye fani ya filamu, Joseph Rushahu 'Bwana Misosi', amevunja ukimya kwa kuachia wimbo mpya uitwao 'Iweje'.
Wimbo huo umefyatuliwa na Bwana Misosi, baada ya kipindi kirefu cha ukimya tangu mwaka jana alipoachia nyimbo mbili za 'Pilato na Game' alioimba na Sir Juma Nature na Fid Q na ule wa 'Mungu Yupo Bize'alioimba na Said Chigunda 'Chegge'.
Akizungumza na MICHARAZO, Bwana Misosi, alisema wimbo huo mpya ameurekodia studio za HM Records zilizopo Kawe na anatarajiwa kuachia hivi karibuni sambamba na video yake aliyoanza kuishuti.
"Kaka nimekamilisha 'ngoma' mpya iitwayo 'Iweje' ambayo nimekamua mwenyewe bila kupigwa tafu na mtu na kwa sasa nakamilisha mipango ya video kabla ya kuachia kwa pamoja itakapokamilika video hiyo," alisema Bwana Misosi.
Msanii huyo alisema wimbo huo kama zilizotanguliwa zitakuwa za kufanyia show tu na wala hana mpango wa kutoa albamu kama alivyofanya mwaka 2004 na 2007.
"Sina mpango wa kutoa albamu, natoa singo tu kuwapa burudani mashabiki wangu sawia na kupata nafasi ya kugonga shoo," alisema.
Aliongeza wakati akiendelea na mchakato wa kupakua video ya wimbo huo wa 'Iweje', pia anaendelea na zoezi la upigaji picha wa filamu mpya ya pili anayotarajiwa kuibuka nayo.
Bwana Misosi , aliyeingia kwenye fani hiyo akiwa na filamu ya 'Mkoba' ambayo ipo njiani kuachiwa mtaani ikiwa imeshirikisha wakali kama Amanda na Mzee Majuto, alisema filamu hiyo mpya ya pili ipo hatua ya mwisho kabla ya kukamilika.

No comments:

Post a Comment