STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, December 5, 2012

UGANDA YAIFUATA KILI STARS NUSU FAINALI TUSKER CHALLENGE 

Chanzo BIN ZUBEIRY 

Wachezaji wa Uganda wakimpongeza Geoffrey Kizito (anayetazama kamera amekumbatiana na Kiiza), baada ya kufunga bao kwanza dakika ya nne dhidi ya Ethiopia katika Robo Fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Tusker Challenge kwenye Uwanja wa Mandela, Namboole mjini Kampala. Uganda ilishinda 2-0 bao lingine likifungwa na Robert Ssentongo dakika ya 60 na kwa ushindi huo, Uganda itamenyana na Tanzania Bara katika Nusu Fainali Alhamisi usiku, mchezo ambao utatanguliwa na Nusu Fainali nyingine kati ya Kenya na Zanzibar.
Ssentongo akisababisha

Kiiza mawindoni

Kipa Samson Asfaw Worku akiwa amedaka mpira, huku beki wake Girma Bekele Debele akimdhibiti Brian Umony kulia

Gotochi Panom Yietch akigombea mpira na Robert Ssentongo kulia

Robert Ssentongo anaondoka na mpira baada ya kumlamba chenga beki wa Ethiopia kulia

Hamisi Kiiza akimtoka Chala Deriba Debala wa Ethiopia

Kiiza, Walusimbi, Wasswa wakicheza na Ssentongo 

Kutoka kulia Hamisi Kiiza na Henry Kalungi wakimpongeza Robert Ssentongo kufunga bao la pili

No comments:

Post a Comment