STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, December 4, 2012

Zuku Tv yazindua huduma mpya ya malipo kwa wateja wao

Meneja wa kampuni ya Wananchi Satellite Ltd, Fadhil Mwasyeba (kushoto) akifafanua jambo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa uzinduzi wa huduma za malipo kwa wateja wao uliofanyika leos asubuhi jiji Dar es Salaam baada ya kampuni hiyo kuingia mkataba na kampuni ya Selcom Wireless Ltd. Anayeonekana kati ni Meneja Uhusiano wa Selcom, Juma Tumaini Mgori.



KAMPUNI ya Wananchi Satellite Ltd inayomiliki televisheni ya kulipia ya Zuku kikishirikiana na kampuni ya Selcom Wireless Ltd zimeingia mkataba wa kuanza kutoa huduma rahisi ya malipo kwa wateja wa televisheni hiyo kwa nchi nzima.
Uzinduzi wa huduma hizo ulifanyika leo jijini Dar es Salaam baada ya viongozi wa pande hizo mbili kusaini mkataba huo mbele ya waandishi wa habari katika hafla fupi iliyofanyika kwenye ukumbi wa Diamond, uliopo  Ubungo.
Meneja wa Wananchi Satellite kwa hapa nchini, Fadhili Mwasyeba alisema wameamua kurahisisha huduma ili kuwapa fursa wateja wao kufanya malipo kwa njia nyepesi na ya haraka tofauti na siku za nyuma.
"Tuna furaha juu ya ushirikiano huo mpya na utakaowajali wateja wetu wa Zuku. Ahadi yetu ni kutoa ufumbuzi rahisi kwa wateja wetu wafanyabiashara na wauzaji na ufumbuzi huui utatuwezesha kufika mbali zaidi ya matarajio ya vwateja wetu." alisema.
Aidha Mwasyeba aliongeza kuwa wakati wakiwarahisishia unafuu wa kulipa malipo ya kila mwezi kwa wateja wao, pia kampuni yao inaendelea na promosheni yao ya kuwazawadia wateja wao iitwayo Zuku Tunakuthamini-Pata Tv Bure'.
Alisema kinachotakiwa kwa wateja kuwaunganisha wateja watano kujiunga na Zuku na kulipia malipo na kisha kujishindia runinga kati ya inchi 22 na wale watakaofikisha idadi ya wateja 10 watanyakua rungina ya inchi 42 na walioungwanishwa nao wakiambulia 'offer' nyingine zinazotolewa na kampuni yao kupitia promosheni hiyo.
Naye Meneja Uhusiano wa Selcom, Juma Tumaini Mgori, alisema kuanza kutoa huduma hiyo kwa wateja wa zuku ni fursa ya kuwapa unafuu wateja wa televisheni hiyo popote walipo nchini kutokana na kampuni yao kuwa na vituo vya malipo zaidi ya 1500.
"Tunajitahidi kufanya kazi kwa ufanisi kwa malipo ya ushirikiano wa kipekee na zuku ili kuwafikia wateja kwa ukaribu zaidi," alisema na kuongeza;
Tuna furaha kufanya kazi na Zuku na tunaamini huu ni mwanzo tu wa ushirikiano wa kibiashara," alisema.
Televisheni ya Zuku inatoa uchaguziu mpana wa stesheni za burudani ikiwa ni pamoja na habari, michezo na sinema, majarida na muziki ikiwa imejumuisha chaneli za kimataifa kama BBC, MTV Base. Sentanta Sports, MGM Movies na nyinginezo ka gharama nafuu kwa ubora na kiwango cha hali ya juu.
Mameneja wa kampuni za Wananchi Satellite Ltd, Fadhil Mwasyeba (kushoto) na Juma Tumaini Mgori wa Selcom Wireless wakibadilishana mkataba waliosaini leo ili kutoa huduma rahisi na ya haraka ya malipo kwa wateja wa Zuku Tv. Uzinduzi huo uliofanyika leo asubuhi jijini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment