STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, January 16, 2013

Azam kwenda Kenya kujifua zaidi

 
BAADA ya kutwaa Kombe la Mapinduzi mwishoni mwa wiki visiwani Zanzibar, Azam FC inatarajiwa kuondoka nchini Alhamisi kwenda Nairobi, Kenya kwa ziara ya wiki moja ya michezo ya kirafiki, kujiandaa na mzunguko wa pili wa Ligi Kuu na Kombe la Shirikisho.
Katibu Mkuu wa Azam FC, Nassor Idrisa ameiambia BIN ZUBEIRY leo kwamba katika ziara hiyo watacheza mechi tatu za kujipima nguvu dhidi ya timu za Sofapaka, AFC Leopards na Gor Mahia kabla ya kurejea nchini Januari 23.
Nassor alisema ziara hiyo ni maalum kwa ajili ya kuiweka sawa timu yao kabla ya kuanza kwa mzunguko wa pili wa Ligi Kuu ya Bara na Kombe la Shirikisho Afrika.
Nassor amesema anaamini timu za Kenya ni nzuri na zitawapa changamoto nzuri kabla ya kuanza kwa mzunguko wa pili wa Ligi Kuu na kuingia kwenye Kombe la Shirikisho.
“Tumekuwa katika programu ndefu ya maandalizi tangu Desemba, tukianzia Kongo (DRC) ambako tulicheza mashindano na kuchukua Kombe, tumetoka tumeingia kwenye Kombe la Mapinduzi tumeshiriki na kuchukua Kombe, na sasa tunakwenda Kenya,”alisema Nassor.
Katibu huyo alisema kikosi kizima cha Azam kitakwenda Kenya kwenye ziara hiyo na baada ya hapo timu itarejea tayari kwa mzunguko wa pili wa Ligi Kuu.
 

IMEHAMISHWA: BIN ZUBEIRY

No comments:

Post a Comment