STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, January 16, 2013

Zahoro Pazi aenda kujaribiwa Afrika Kusini

Zahoro Pazi akiwa kando ya 'mkoko' wake hivi karibuni mitaa ya Temeke Maduka Mawili

MSHAMBULIAJI wa zamani wa timu za Mtibwa na Azam aliyekuwa ametua JKT Ruvu kwa mkopo, Zahoro Pazi, ameondoka nchini juzi usiku kuelekea Afrika Kusini kufanya majaribio ya kucheza soka la kulipwa katika klabu ya Ligi Kuu ya Bloemfotein Celtic.
Akizungumza na MICHARAZO muda mchache kabla ya kupaa kuelekea nchini humo, Pazi alisema kuwa safari yake imefanywa na wakala wake ambaye hakupenda kumtaja jina na kwamba mipango hiyo ilikuwepo tangu mwishoni mwa mwaka jana.
Pazi, alisema kwamba klabu hiyo ya Bloemfotein Celtic inayoshiriki Ligi Kuu ya Afrika Kusini, ilivutiwa naye kupitia michuano ya Kombe la Kagame pamoja na kutuma maskauti wao walipoenda DR Congo kushiriki michuano ya Kombe la Hisani.
"Ndoto zangu za kucheza soka la kulipwa baada ya kukwama mara mbili Ujerumani na Umangani naona zinaelekea kuwa kweli kwani nimeitwa na klabu ya Bloemfotein Celtic kwa ajili ya kufanyiwa majaribio," alisema Pazi.
Pazi, mtoto wa kipa nyota wa zamani wa kimataifa wa Tanzania aliyewahi kutamba na timu za Pilsner, Simba, Taifa Stars na El Merreikh ya Sudan, Idd Pazi 'Father' alisema ana imani kubwa ya kufanya vema majaribio yake.
"Sina hofu yoyote na safari yangu hii, kama niliweza kuivutia Kaiserslautern ya Ujerumani sidhani kama nitashindwa Afrika Kusini muhimu niombeeni dua Mungu anifanyie wepesi," alisema Pazi.
Kinda hilo lililozaliwa Julai 4, 1989 akiwa mtoto wa mwisho kati  ya watoto wawili wa Idd Pazi, alisema majaribiuo yake amedokezwa yatakuwa ya wiki moja na kama kutakuwa na lolote la ziada atalifahamisha NIPASHE akiwa nchini humo.
***

No comments:

Post a Comment