STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, January 16, 2013

Mbio za uchaguzi wa TFF zapambamoto

Michael Wambura



ALIYEKUWA Katibu Mkuu wa Chama cha Soka Tanzania (FAT sasa TFF), Michael Wambura na kiongozi wa zamani wa klabu iliyokuwa Ligi Kuu ya Moro United ‘Chelsea ya Bongo’, Muhsin Balhabou ni miongoni mwa wadau wa soka walichukua fomu jana kuwania nafasi mbalimbali za uongozi ndani ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).
Wambura amechukua fomu kuwania umakamu wa rais huku Balhabou akiwania nafasi ya ujumbe katika kamati ya uchaguzi ya TFF. Uchaguzi huo utafanyika Februari 24 jijini Dar es Salaam
Tayari wagombea wengine wawili, Makamu wa Pili wa Rais anayemaliza muda wake, Ramadhan Nassib na Mjumbe wa Kamati ya Utendaji inayomaliza muda, Wallace Karia wameshachukua fomu za kuwania nafasi anayoiwania Wambura.
Wanamichezo wengine waliochukua fomu jana ni pamoja na Mbasha Matutu, Salum Chama, Titus Osoro na Zafarani Damoder ambao wote wanawania pia nafasi za ujumbe wa kamati ya utendaji ya TFF.
Wagombea wengine waliojitokeza kuchukua fomu za kuwania ujumbe ni Salum Chama anayewania kupitia Kanda ya Kagera na Geita, Mugisha Galibona, Samuel Nyalla, Titus Osoro na Vedastus Lufano (Mara na Mwanza), Epaphra Swai na Mbasha Matutu (Shinyanga na Simiyu), Charles Mugondo, Elly Mbise na Twahili Njoki (Arusha na Manyara) huku Yusuph Kitumbo (Kigoma na Tabora).
Ayubu Nyaulingo, Nazarius Kilungeja na Selemani Kameya (Katavi na Rukwa) na James Mhagama (Njombe na Ruvuma), Athuman Kambi (Lindi na Mtwara), Hussein Mwamba na Stewart Masima (Dodoma na Singida), Farid Nahdi (Morogoro na Pwani), Khalid Mohamed (Kilimanjaro na Tanga) na Muhsin Balhabou, Shaffih Dauda na Zafarani Damoder (Dar es Salaam).
Taarifa iliyotolewa jana na Afisa Habarin wa TFF, Boniface Wambura, imeeleza kuwa jumla ya waliochukua fomu hadi sasa ni watu 26, lakini idadi hiyo ni ya wale wanaochukua fomu hizo katika ofisi za TFF. Fomu hizo huchukuliwa pia kupitia tovuti ya TFF (www.tff.or.tz) na mwisho wa kuchukua na kuzirejesha ni keshokutwa Ijumaa, saa 10:00 jioni.
Mwaka 2004, Wambura pamoja na aliyekuwa Mwenyekiti wa FAT, Muhiddin Ndolanga, waliangushwa na Tenga lakini mwaka 2008, Wambura alijitosa tena katika nafasi ya Makamu wa Kwanza wa Rais lakini jina lake lilienguliwa kwa maelezo kwamba hakuwa na sifa ya uadilifu.
Hata hivyo, mwaka jana Wambura akiwa anawania nafasi ya uenyekiti wa Chama cha Soka cha Mkoa wa Mara (FAM), jina lake lilienguliwa na baada ya kukata rufaa lilirejeshwa lakini muda wa uchaguzi ulikuwa umeshamalizika na hivyo alishindwa kuwania cheo hicho kama alivyodhamiria.
Juzi, Tenga alitangaza wazi kwamba hatawania tena cheo hicho na hivyo kuwapunguzia 'presha' wale waliokuwa wakihofia kutwaa fomu za kuwania uenyekiti wa shirikisho hilo kwa sababu yake.
Katika hatua nyingine, Said Mohamed amechukua fomu ya kuwania umakamu mwenyekiti wa Bodi ya Ligi Kuu (TPL Board).

No comments:

Post a Comment