STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, January 31, 2013

Balotelli ilibidi tu aondoke - Mancini


Kocha Mancini akiwa na Balotelli wakipeana majukumu wakati walipokuwa pamoja Manchester City

KOCHA wa Manchester City, Roberto Mancini amesema kuondoka kwa Mario Balotelli kwenda AC Milan kunaifanya timu yake ipungukiwe wachezaji.
Sare yao ya 0-0 dhidi ya QPR usiku wa kuamkia jana iliwaacha mabingwa wakiwa hatarini kupitwa zaidi na vinara Manchester United, ambao usiku wa kuamkia leo walitarajiwa kucheza dhidi ya Southampton.
"Ni ngumu kwa sababu nimempoteza mchezaji mmoja muhimu na ambaye angekuwa muhimu katika mechi 14 zijazo," alisema Mancini.
"Lakini ilikuwa ni muhimu kwa Mario kurejea Italia, kurejea kwenye familia yake na kuchezea Milan."
Mancini anaamini kwamba Balotelli amefanya kazi "nzuri sana" katika miaka yake miwili na nusu akiwa na Man City, ingawa amekubali kwamba msimu huu ulikuwa mgumu zaidi kwa mshambuliaji huyo.
Mancini pia haraka alikanusha mtazamo kwamba kuondoka kwa Balotelli kumetokana na ugumu wa kumdhibiti mshambuliaji huyo mtata.
"Hapana, hapana, hapana, siyo kwangu," alisema. "Kwangu mimi, Mario alikuwa kama mwanangu mwingine.
"Mario yuko hivyo lakini anaweza kukufadhaisha wakati mwingine.
"Klabu imeniambia kwamba imepokea ofa kutoka Milan. Nilizungumza na Mario na nadhani alitaka uhamisho huu.
"Nadhani kwake kucheza miaka mitatu England na kisha kurejea Italia itakuwa ni jambo zuri kwake."
Balotelli alitambulishwa rasmi jana na klabu yake mpya ya AC Milan akikabidhiwa jezi yenye namba kama alivyokuwa akiitumia alipokuwa City, 45.

No comments:

Post a Comment