STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, January 31, 2013

Madrid yaidindia Barca Kombe la Mfalme

Cesc Febregas akishangilia bao katika pambano la jana la El Clasico
MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu ya Hispania, Real Madrid usiku wa kuamkia leo iliikomalia vinara wa ligi hiyo, Barcelona kwa kulazimishwa sare ya bao 1-1 katika pambano la nusu fainali ya kwanza ya Kombe la Mfalme katika pambano lililochezwa kwenye uwanja wake wa nyumbani, mjini Madrid.
Ikicheza bila baadhi ya nyota wake kutokana na kutumikia adhabu na kuwa majeruhi, Real Madrid iliibana Barca na kwenda nao mapumziko wakiwa nguvu sawa bila kufungana.
Kipindi cha pili kilianza kwa kasi na Barcelona kuwashtua wenyeji wao kwa kujipatia bao la kuongoza lililofungwa dakika ya 50 na kiungo Cesc Fabregas akimalizia kazi nzuri ya Lionel Messi.
Timu hizo zilizoenda kushambuliana na kufanya kosa kosa kadhaa na kwenye dakika ya 81, wenyeji walifanikiwa kusawazisha bao hilo kupitia kwa Raphael Varane aliyemaliza kazi murua ilioyofanywa na Mjerumani Mesut Ozil.
Wapinzani hao wa jadi wa nchini Hispania wanatarajiwa kurudiana mwishoni mwa mwezi Februari, ambapo ndiyo itaamua hatma ya timu ipi itinge fainali za michuano hiyo kuungana na mshindi kati ya Sevilla na Atletico Madrid ambazo nufa fainali yao ya kwanza inatarajiwa kuchezwa kesho mjini Madrid kabla ya kwenda kurudiana nyumbani kwa Sevilla.
Katika pambano hilo la El Clasico lililoshuhudia Barcelona ikiwatumia wachezaji wake waliokuwa nje kwa muda mrefu kwa majereha, wachezaji sita, watatu kila upande wakionyeshwa kadi za njano kwa makosa mbalimbali.

No comments:

Post a Comment