STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, January 31, 2013

BREAKING NEWS: DIZUMBA WA MAJIMAJI AFARIKI

HABARI zilizotufikia muda huu zinasema kuwa aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa klabu ya Majimaji Songea inayojiandaa na duru la pili la Ligi Daraja la Kwanza Tanzania Bara, Ahmed Dizumba amefariki dunia.
Taarifa zilizopatikana asubuhi hii ambazo MICHARAZO inaendelea kuzifuatilia kwa ukaribu zinasema Dizumba amefariki usiku wa kuamkia leo na anatarajiwa kuzikwa leo mjini Songea.
Kwa yeyote mwenye taarifa zaidi anaweza kutupenyezea, juu ya msiba huu ulioikumba Majimaji ikiwa katika harakati za kuanza duru la pili la ligi daraja la kwanza kuwania kurejea ligi kuu.
Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa na TFF, Majimaji imepangwa kuanza utepe wa duru hilo kwenye uwanja wake wa Majimaji Songea kuvaana na Kurugenzi mechi ya kundi A.

No comments:

Post a Comment