STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, January 7, 2013

KUMEKUCHA MISS UTALII TANZANIA


KAMBI ya warembo watakaoshiriki fainali za shindano la urembo la Utalii, Miss Utalii Tanzania, inatarajiwa kuanza rasmi Jumamosi ijayo ikishirikisha warembo walioshika nafasi mbili za juu ya mashindano ya ngazi ya mkoa.
Rais wa Miss Utalii Tanzania, Gideon Chipungahelo 'Chipps' aliiambia MICHARAZO kambi hiyo itakuwa ya siku 21 kabla ya kufanyika kwa kinyang'anyiro hicho mwishoni mwa mwezi huu jijini Dar es Salaam.
Chipps aliwataja warembo watakaoingia kambini tayari kuwania taji hilo la Tanzania na tuzo nyingine 28 zitakazowaniwa kuwa ni pamoja na Rose Godwin (Arusha), Irene Thomas, Sophia Yusuph na Ivon Stephen wote wa Dar.
Wengine ni Erica Elibariki (Dodoma), Jamia Abdul (Geita), Debora J. Mwansepeta (Iringa), Anna Pogaly (Kilimanjaro), Zena Sultan (Kigoma), Asha Ramadhani (Katavi), Joan John (Lindi), Doreen Bukoli (Mara), Dayana Joachim (Mbeya) na Jessica Rugalabamu wa Mwanza.
Warembo wengine ni Halima Suleman (Mtwara), Hadija Saidi (Morogoro), Mary Rutta (Manyara), Paulina Mgeni (Njombe), Anganile Rogers (Rukwa), Furaha Kinyunyu (Ruvuma), Neema Julius (Singida), Flora Msangi (Simiyu), Lightness Kitua (Shinyanga), Magreth Malale (Tabora) na Sarafina Jackson wa Tanga.
Wawakilishi wa vyuo wakaoshiriki kinyang'anyiro hicho ni Irene Richard Makoye na Hawa Nyange.
Tuzo zitakazowaniwa na warembo hao mbali na taji litakalompa mshindi uwakilishi wa nchi katika shindano la kimataifa ni pamoja na tuzo za heshima za Jamii, Elimu ya Jamii, Afya ya Jamii, Utalii, Utamaduni, Uchumi, Miundo Mbinu ya Utalii, Uwekezaji, Madini na maliasili mbalimbali za taifa.

No comments:

Post a Comment