STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, January 7, 2013

Suarez afunga bao la utata na kuivusha Liverpool Kombe la FA

HATUA KWA HATUA YA BAO LA UTATA LA SUAREZ JANA
Suarez akijitengenezea vizuri mzuri kwa mkono
Amefanikiwa na sasa anaelekea kufunga bao

Akimtoka kipa aliyejaribu kumzuia
Kazi imekuwa nyepesi anafunga kilainii..huku Mansfield wakiinua mikono wakilalamikia bao hilo

Anashangilia na wenzake

Anaubusu mkono wake kwa kazi nzuri uliofanya

 

NYOTA wa timu ya Liverpool, Luis Suarez, jana akitokea benchi alitengeneza bao kwa mkono kisha kufunga na kuivusha timu yake kwenye michuano ya Kombe la FA nchini England.

Bao hilo ambalo tukio la kutengenezwa na mkono halikuonwa na mwamuzi wa pambano hilo la raundi ya tatu ya michuano hiyo iliisaidia kuipa Liverpool ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya

Mansfield Town.
Raia huyo wa Uruguay ambaye anakumbukwa na Waafrika kwa kulizuia bao la Ghana katika Fainali za Kombe la Dunia 2010, alifunga bao hilo katika dakika ya 59 dakika tano tangu aingie dimbani kuchukua nafasi ya Daniel Sturridge, aliyetangulia kufunga bao la mapema.
Wenyeji Mansfield waliolalamikia tukio hilo, walipata bao la kufutia machozi dakika ya 80 kupitia Matt Green, ambalo halikuwasaidia kutong'oka kwenye michuano hiyo ambayo pia jana ilishuhudiwa Arsenal wakilazimishwa sare ya 2-2 ugenini na Swansea City.
Arsenal ilielekea kushinda pambano hilo baada ya kutoka nyuma ya bao 1-0 mara kipindi cha pili kilipoanza baada ya dakika 45 za kwanza kwenda mapumziko bila kufungana na kufunga mabao mawili dakika 10 za mwisho wa mchezo huo kabla ya kujisahau na Swansea kusawazisha zikiwa zimesalia dakika tatu.
Michu alianza kuiandikia Swansea bao dakika ya 51 kabla ya Lucas Podolski kusawazisha dakika ya 81 na Kieran Gibbs kufunga bao la pili dakika mbili baadae na wakati wengi wakiamini Arsenal imepita kwa raundi ya nne,  Danny Graham kusawazisha bao hilo na kuzifanya timu zao sasa kurudiana tena ili kufuzu hatua ijayo itakayoanza Januria 26.

Amefanikiwa na sasa anaelekea kufunga bao

No comments:

Post a Comment