STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, January 7, 2013

Sepp Blatter apinga kitendo kilichofanywa na Boateng, AC Milan

Rais wa FIFA, Sepp Blatter

RAIS wa Shirikisho wa Soka Duniani, FIFA, Sepp Blatter ameponda kitendo cha nyota wa AC Milan, Kevin Prince Boateng kuamua kususa pambano lao la kirafiki la wiki iliyopita dhidi ya timu ya daraja la chini ya Pro Patria, akidai haiwezi kuvumiliwa.
Blatter alinukuliwa jana akiwa Dubai kwenye zira ndefu ya Mashariki na Kati, akisema kuwa kilichofanywa na Boateng na timu yake ya Milan haiwezi kusaidia kumaliza ubaguzi zaidi ya kuongeza tatizo, iwapo kila timu au kila mchezaji watakuwa wakiamua kususa mechi kwa kufanyiwa vitendo kama hivyo.
"Sidhani kama kuondoka uwanjani ndio suluhisho la tatizo, inaweza kutumiwa vibaya na timu nyingine hasa kama timu imefungwa katika pambano hilo," alinukuliwa Bletter.
Alisema wanasubiri taarifa toka Shirikisho la Soka la Italia kujua kitu gani kilichotokea, ingawa alisisitiza kuwa pamoja na kwamba FIFA inapinga vitendo vya ubaguzi, lakini pia haiungi mkono tabia ya kususia mechi vinapotokea vitendo kama hivyo wakati wa mechi.
Kevin Prince Boateng kiungo wa AC Milan

Boateng nyota wa zamani wa timu ya taifa ya Ghana, Black Stars, aliamua kutoka uwanjani baada ya kufanyiwa vitendo vya kibaguzi na mashabiki wa Pro Patria katika mechi ya kirafiki iliyochezwa Alhamis iliyopita ambapo licha ya kubembelezwa aligoma kufuta msimamo wake na kusababisha mechi hiyo kuvunjika.
Jana Jumapili wachezaaji wa timu hiyo ya Milan, walitinga uwanjani katika pambano lao la Seria A wakiwa na jezi zenye maandishi ya kupinga ubaguzi wa rangi ambapo timu hiyo ilipata ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Siena.
Vitendo vya kibaguzi dhidi ya wachezaji wenye asili ya Afrika kwa mataifa ya Ulaya vimekuwa vikizidi kushamiri kwa siku za karibuni, baadhi vikifanywa na wachezaji wenyewe kwa wenyewe na wakati mwingine vikifanywa na mashabiki kama ilivyotokea kwa Boateng.


Wachezaji wa AC Milan wakiwa wamevaa jezi zinazopinga ubaguzi wa rangi kabla ya mechi yao ya Seria A dhidi ya Siena jana
Hata hivyo pamoja na FIFA na FA za nchi mbalimbali kuvipinga vitendo hivyo na kutoa adhabu kwa wahusika bado havijaleta tija hasa kutokana na adhabu zake kuonekana nyepesi kuliko ukubwa wa jambo hilo.

No comments:

Post a Comment