STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, February 11, 2013

NIGERIA BINGWA MPYA WA AFRIKA YAIZIMA BURKINA FASO


Cup of joy: A jubilant Nigeria squad hoist the Africa Cup of Nations trophy aloft for the third time
Wachezaji wa Nigeria wakishangilia Kombe lao la Mataifa ya Afrika baada ya kuifunga Burkina Faso kwenye Fainali nchini Afrika Kusini jana.Fancy seeing you again: Nigeria coach Stephen Keshi grabs the Africa Cup of Nations trophy after winning the competition as a player in 1994
Kocha wa Nigeria, Stephen Keshi akiwa ameshika Kombe ambalo awali alitwaa akiwa mchezaji mwaka 1994Warm welcome: FIFA president Sepp Blatter was made to feel at home in Johannesburg
Rais wa FIFA, Sepp Blatter wa pili kutoka kulia alikuwepo Johannesbug jana, chini mashabiki wakiwa na bango na kuonyesha upendo wa Waafrika kwake
Warm welcome: FIFA president Sepp Blatter was made to feel at home in South Africa
Winner: Sunday Mba is congratulated by Nigeria team-mates after firing the only goal of the game
Sunday Mba akipongezwa na wenzake kwa kufunga bao la ubingwa
No holds barred: Burkina Faso's Mady Panandetiguiri clashes with Nigeria keeper Vincent Enyeama
Mchezaji wa Burkina Faso, Mady Panandetiguiri akivaana na kipa wa Nigeria, Vincent Enyeama
Outnumbered: Nigeria's Victor Moses scraps for possession with Burkina Faso's Bakary Kone (centre), Mohamed Koffi (back) and Djakaridja Kone (right)
Mchezaji wa Nigeria, Victor Moses akipambana na ukuta Burkina Faso, Bakary Kone (katikati), Mohamed Koffi (nyuma) na Djakaridja Kone (kulia)

NCHI ya Nigeria jana usiku ilifanikiwa kutwaa ubingwa wa Afrika ikiwa ni kwa mara ya kwanza tangu miaka 19 na taji la tatu kwa nchi hiyo baada ya kuifunga Burkina Faso bao 1-0 katika fainali kali iliyopigwa kwenye Uwanja wa FNB(Soccer City), Johannesburg, Afrika Kusini.
Shujaa wa Nigeria kwa mechi ya jana alikuwa ni Sunday Mba aliyefunga bao hilo pekee la ushindi dakika ya 40, baada ya kutokea purukushani kwenye lango la Burkina Faso.
Burkina Faso ambayo hiyo ndiyo fainali yake ya kwanza kucheza tangu ilipoanza kushiriki michuano hiyo, ilipigana kutaka kurudisha bao hilo, lakini bahati haikuwa yao na hivyo kujikuta wakijifuta machozi kwa kushika nafasi ya pili.
Nigeria ilitwaa taji la michuano hiyo mwaka 1980 na 1994 na baada ya hapo ilikuwa ikishuhudia mataifa mengine yakinyakua kabla ya mwaka huu ikiwa chini ya kocha mzawa Stephen Keshi aliyenyakua taji la mwisho mwaka 1994, kuibebesha taji hilo akiweka rekodi ya kuwa kocha wa 15 mzawa kubebea taji hilo dhidi ya 14 ya makocha wa kigeni wa nchi mbalimbali katika michuano hiyo ya Afrika.

No comments:

Post a Comment