STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, February 24, 2013

SIMBA YAVUTWA SHARUBU, YALALA TENA NA MTIBWA

KIkosi cha Simba kilicholala leo kwa Mtibwa Sugar


Mtibwa Sugar walioendeleza ubabe kwa Simba leo uwanja wa Taifa (Picha Zote:Francis Dande)

MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Simba jioni ya leo imeendelea kuwa mteja wa Mtibwa Sugar baada ya kufungwa bao 1-0 katika pambano kali lililochezwa kwenye uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Mtibwa ilijipatia bao hilo la pekee katika dakika ya 19 ya mchezo kupitia kwa beki wake mahiri, Salvatory Ntebe bao lililoihakikishia timu yake kuvuna pointi zote sita kwa msimu mbele ya Simba.
Kwani katika pambano lao la duru la kwanza Simba ilikubali pia kichapo cha mabao 2-0 na kupelekea kuibuka kwa mtafaruku toka kwa wanachama wa klabu hiyo waliokuwa wakishinikiza nahodha na kipa tegemeo wa timu hiyo Juma Kaseja na baadhi ya viongozi kujiuzulu kwa madai waliifanyia hujuma.
Katika pambano hilo, beki kisiki wa Simba Juma Nyosso alijikuta akitolewa nje na mwamuzi Kidiwa dakikia za lala salama, wakati tayari jahazi la timu yake likielekea kuzama mbele ya Mtibwa ambayo katika mechi yake ya mwisho ilikumbana na kipigo cha mabo 4-1 toka kwa Azam.
Kipigo hicho kimeiacha Simba kuendelea kusalia kwenye nafasi yake ya tatu nyuma ya Azam waliolala bao 1-0 jana kwa vinara wa ligi hiyo Yanga wanaoongoza msimamo kwa sasa wakiwa na pointi 39.
Mabingwa hao watetezi wa ligi kuu wanatarajiwa kuondoka nchini katikati ya wiki hii kuelekea Angola kwa ajili ya pambano lake la marudiano ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya wenyeji wao Libolo ambao walishinda meechi ya wali kwa bao 1-0.
Kocha Msaidizi wa Simba alizungumza baada ya pambano hilo akidai wanakubali matokeo kwanu kufungwa ni sehemu ya matokeo matatu ya soka, huku akiahidi kujipanga kwa ajili ya mechi zao nyinginee za ligi mara watakaporejea toka Angola.

No comments:

Post a Comment