STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, February 24, 2013

CHELSEA HOI KWA MAN CITY, NEWCASTLE YATAKATA



Lampard (8) akikosa penati iliyopanguliwa na kipa Joe Hart


WAKATI Newcastle United ikitakata nyumbani kwake kwa kuigagadua Southampton kwa mabao 4-2, vijana wa Rafa Benitez wamejikuta wakiangukia pua ugenini kwa kunyukwa na mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya England, Manchester City mabao 2-0 katika pambano kali lililochezwa jioni hii.
Chelsea walionyesha kuhimili vishindo vya wenyeji wao na kulazimisha kwenda mapumziko wakiwa nguvu sawa kwa kutofunga bao lolote.
Hata katika kipindi cha pili, Chelsea walionyesha uhai kwa kuwakimbiza wapinzani wao na kufanikiwa kupata penati iliyoshindwa kufungwa na mkongwe Frank Lampard kabla ya Yaya Toure kuifungia wenyeji bao dakika ya 63.
Dakika tano kabla ya pambano hilo kumalizika shuti kali la kushtukiza la Carlos Tevez liliwanyong'onyesha Chelsea kwani liliwavunja nguvu za kuweza kusawisha bao na kuambulia sare.
Katika pambano jingine lililochezwa leo, Newcastle United wakiwa nyumbani waliishindilia wageni wao Southampton kwa mabao 4-2.
Wageni waliwashtua wenyeji wao wa kuandika bao la kuongoza dakika tatu tu ya mchezo kupitiaMorgan Schneiderlin kabla ya Mousa Sissoko kusawazisha dakika ya 33 na na nyota wa Senegal, Papiss Demba Cisse kuongeza la pili dakika ya 42 naa kufanya hadi mapumziko Newcastle kuongeza bao 2-1.
Kipindi cha pili kilianza kwa wageni kusawazisha bao kupitia Rickie Lambert  kabla ya Yohan Cabaye kufunga bao la tatu la Newcastle dakika ya 67 na dakika ya 79 beki wa Southampton, Jos Hooiveld kujifunga na kuihakikishia wenyeji ushindi huo mnon0.
Ligi hiyo inatarajiwa kuendelea tena kwa mchezo mmoja tu, West Ham United kuikaribisha Tottenham Hotspur ambayo itakuwa inafukuzia kukalia nafasi ya tatu baada ya leo Chelsea kudorora mbele ya Manchester City.

No comments:

Post a Comment