STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, February 26, 2013

Tottenham Hotspur yaing'oa Chelsea, Gareth Bale awa shujaa

Tottenham Hotspur's Gareth Bale celebrates scoring his side's first goal against West Ham United on February 25, 2013
Gareth Bale (kulia) akishangilia bao na wachezaji wenzake wa Tottenham jana

LICHA ya kucheza ugenini, timu ya Tottenham Hotspur usiku wa kuamkia leo imefanikiwa kuishusha kwnye nafasi ya tatu Chelsea baada ya kupata ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya wenyeji wao West Ham United katika mechi pekee ya Ligi Kuu ya England.
Mabao mawili ya nyota Gareth Bale na moja ya mtoa benchi, Gylfi Sigurdsson iliotosha kuwapa vijana wa Andre Villa Boas, kuzoa pointi tatu na kufikisha jumla ya pointi 41 mbili zaidi ya Chelsea ambayo juzi ililala kwa Machester City na kuiporomosha hadi nafasi ya nne.
Bale alianza kufungua pazi kwa Tottenham dakikia ya 13 kabla ya Andy Carroll kusawazisha kwa mkwaju wa penati dakika ya 25 na kufanya hadi  mapumziko matokeo yawwe bao 1-1.
Kipindi cha pili Joe Cole aliiongezea wenyeji bao la pili katika dakika ya 58 kabla ya mtokea benchi, Sigurdsson kufunga bao la kusawazisha kwenye dakika ya 76 na wakati wengi wakiamini matokeo ya mchezo huo ni sare, Bale akapachika bao la ushindi dakika ya 90.

No comments:

Post a Comment