STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, April 14, 2013

Man City yainyoa Chelsea na kuifuata Wigan fainali FA Cup

Kun Aguero aliyeifungia Man City bao la pili

Vincent Kampany akichuana na Torres

MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu ya England, Manchester City muda mfupi uliopita imefanikiwa kutinga fainali ya Kombe la FA baada ya kuinyuka Chelsea kwa mabao 2-1 na kuifuata Wigan Athletic iliyotangulia katika hatua hiyoi tangu jana.
Chelsea ilijikuta ikienda mapumziko katika pambano hilo lililochezwa kwenye uwanja wa Wembley, Londoni ikiwa nyuma kwa bao 1-0, lililofungwa na Samir Nasir katika dakika ya 35.
Sergio kun Aguero aliiandikia Manchester City bao la pili dakika mbili baada ya kuanza kipindi cha pili na kuifanya timu yake katika mchezo huo wa nusu fainali kucheza kwa kujiamini zaidi.
Demba Ba, alifutia machozi Chelsea kwa kutumbukiza bao pekee ambalo halikuwasaidia kitu katika dakika ya 66 na kufanya hjadi dakika ya mwisho Manchester City kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 na hivyo kusubiri pambano la fainali dhidi yake na Wigan iliyoing'oa Milwall jana kwa mabao 2-0.

No comments:

Post a Comment