STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, April 14, 2013

WAWILI WAFA KATIKA AJALI KAGERA


 

Magari yaliyohusika na ajali hiyo iliyotokea jana jioni huko Ngara, Kagera

Watu wawili wamefariki dunia  papo hapo na wengine wawili kujeruhiwa baada ya gari aina ya Mercedec benz lenye namba ya usajili T 908 ABZ semitrailer lililokuwa ikitokea nchini Burundi, kuacha njia leo(April 13,2013) muda wa saa 12 jioni na kupinduka katika eneo la Kumuyange nje kidogo ya mji wa Ngara mkoani Kagera.

Kamanda wa Polisi wilaya ya Ngara  Abel Mtagwa amewataja watu hao waliofarki katika ajali hiyo kuwa ni Edward Filimon alie kuwa akiendesha pikipiki yake yenye namba za usajiri T 756 BZJ na abiria wake ambae hadi sasa haja fahamika jina lake.
Kamanda Mtagwa amewataja majeruhi wa ajari hiyo kuwa ni Dereva wa gari hilo Hajji Omary Ibrahim(29) mkazi wa gongolamboto jijini Dar es salaam na tingo wake aliyejulikana kwa jina la Kambi simba(40).
Kamanda Mtagwa ameongeza kuwa katika ajal i hiyo nyumba moja mali ya Bi.Bibiana John (58) imegongwa na gari hilo na kuharibika.
Aidha Kamanda Mtagwa amesema kuwa chanzo cha ajari hiyo ni  gari hilo kufeli  mfumo wa Breki  jambo ambalo Dereva wake alishindwa kulimudu kuliendesha ndipo lilipanda mtaro na kubomoa nyumba hiyo. 
 
Aidha Majeruhi wa Ajali hiyo wamelazwa katika Hospitali ya Murugwanza wilayani Ngara.
 
CHANZO:MWANA AFRIKA

No comments:

Post a Comment