STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, April 21, 2013

Yanga yakihakikishia ubingwa wa 23 Tanzania Bara

Kikosi cha Yanga
NI Miujiza tu itakayoizuia Yanga kuwa Mabingwa Wapya msimu huu baada ya jioni ya leo kuifumua maafande wa JKT Ruvu kwa mabao 3-0 katika pambano pekee la Ligi Kuu Tanzania Bara.
Ushindi huo umnewafanya vinara hao kufikisha pointi 56 ambazo zinawaweka katika nafasi nzuri ya kutwaa taji lake la 23 la Ligi Kuu kutokana na ukweli ni Azam pekee inayoweza kuzifikia pointi hizo ikishinda mechi zake zote, wakati Yanga ikiwa bao na mechi mbili mkononi.
Hata hivyo Yanga inawabidi wasubiri kuanza kusherekea ubingwa huo ambao ni dhahiri ni wao msimu huu mpaka jumamosi kusikilizia mechi ya Azam na Coastal Union itakayochezwa mjini Tanga.
Iwapo Azam italazimishwa sare yoyote basi itatoa fursa ya wana Jangwani kusherehekea ubingwa wa 23 wa Ligi hiyo bila kushuka dimbani.
Mabao yaliyoihakikishia Yanga ushindi huo na kuifanya ilishike kombe la ubingwa kwa mkono mmoja, yalitupiwa kambani na Simon Msuva dakika moja kabla ya mapumziko.
Hamis Kiiza Diego aliiandikia Yanga bao la pili kwa kuunganisha kwa kichwa mpira wa adhabu ndogo uliopigwa na David Luhende katika dakika ya 58.
Kiungo wa kimataifa wa Tanzania, Nizar Khalfan aliiongezea Yanga bao la tatu kwenye dakika ya 62 na kuwafanya maafande wa JKT Ruvu kupoteza dimbani.
Kipigo hicho cha leo kimezidi kuiweka pabaya JKT Ruvu ambayo inanolewa na kocha Kennedy Mwaisabula aliyechukua nafasi ya Charles Kilinda katika eneo la hatari la kushuka daraja.
Timu hiyo iliyopo nafasi ya 11 ikiwana pointi 23 inahitajika kushinda mechi zake tatu zilizosalia iwapo inataka kuepuka kushuka daraja.

Maafande hao wamesaliwa na mechi dhidi ya African Lyon mechi itakayochezwa Jumatano kabla ya kuvaana na Prisons Mbeya kisha kumalizia na Mtibwa Sugar.

 Msimamo Kamili wa Ligi Kuu baada ya mechi ya leo:
                                   P      W     D     L     Gf     Ga     Gd    PTS
1.  Young Africans     24     17     5     2     44     13     +31     56
2. Azam                      23     14     5     4     41     19     +22     47    
3. Kagera Sugar          23     11     7     5     26     18      +8      40     
4.  Simba                     22      9      9     4     32     21     +11     36
5.  Mtibwa Sugar         24      9      9     6     27     24      +3      36   
6. Coastal Union          23      8      9     6     23     20     +3      33    
7.  Ruvu Shooting        23      8      6     9     21     22      -1      30     
8.  JKT Oljoro FC        24      7      7     10   22     28      -6      28     
9. Tanzania Prisons      24      6      8     10   14     21      -7      26    
10.JKT Mgambo          23      7      4     12   15     23      -8      25       11.Ruvu Stars              23      6      5     12    19     37     -18     23
12. Toto Africans         25     4     10     11    22     33     -11     22
13.  African Lyon        23     5       4     14     16     35     -19     19
14. Polisi Morogoro     23     3     10     10     11     21     -10     19

No comments:

Post a Comment