STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, April 21, 2013

Suarez awazima Chelsea na kuiokoa Liverpool isiadhiriwe nyumbani


http://l.yimg.com/iu/api/res/1.2/xe0Me6hmQ6lkB64ccOBXnQ--/YXBwaWQ9eXZpZGVvO2NoPTMwMDA7Y3I9MTtjdz0xOTUwO2R4PTE4MDtkeT0xO2ZpPXVsY3JvcDtoPTEwMDA7cT03MDt3PTY1MA--/http://media.zenfs.com/en_us/News/gettyimages.com/liverpool-v-chelsea-premier-league-20130421-094053-652.jpg
Suarez akiwa sambamba na beki Branislav Ivanovic katika mechi yao ya leo

Chelsea walipokuwa wakishangilia nao lao la pili

BAO la dakika za jioni kabisa lilililofungwa na kinara wa mabao wa Ligi ya England, Luis Suarez imeiwezesha Liverpool kuepuka kipigo cha nyumbani mbele ya Chelsea kwa kulazimisha sare ya 2-2.
Suarez alifunga bao hilo dakika ya sita ya nyongeza za pambano hilo huku Liverpool wakiwa nyuma kwa muda mrefu kw mabao 2-1 na kuzima shamrashamra za vijana wa kocha wao wa zamani  Rafael Benitez.
Chelsea walianza kuwashtukiza wenyeji wao kwa bao la dakika ya 26 kupitia Oscar aliyefunga kwa kichwa akiunganisha krosi nzuri ya Juan Mata, bao lililodumu hadi wakati wa mapumziko.
Kipindi cha pili kilianza kwa kasi kwa wenyeji Liverpool kuandika bao la kusawazisha kupitia nyota wa zamani wa Chelsea, Daniel Strurridge aliyemalizia kazi murua ya Suarez, lakini dakika chache baadaye
Edin Hazard aliifungia Chelsea bao la pili kwa mkwaju wa penati bada ya Suarez kuunawa mpira wakati wa harakati za kulilinda lango lao na kufanya matokeo kuwa 2-1.
Hata hivyo shujaa huyo wa Uruguay na kinara wa orodha wa wafungaji katika ligi hiyo alipowatibulia Chelsea ushindi ambao ungewang'oa Arsenal kwenye nafasi ya tatu kwa kufunga bao la kusawazisha dakika hizo za nyonyeza kwa kumalizia pasi ya Sturridge.
Kwa matokeo hayo ya Chelsea imeendelea kusalia nafasi ya nne ikiwa na pointi 62 wakati Liverpool wameongeza pointi zaidi na kufikisha  51 ikisalia nafasi ya 7 nyuma ya Everton.

No comments:

Post a Comment