STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, May 9, 2013

Adolph Mbinga aanze mambo Sikinde

Adolf Mbinga akiwa kazini


NA MWANDISHI WETU
WASHABIKI wa muziki waliohudhuria onyesho la Jumapili la bendi hiyo lililofanyika kwenye ukumbi wa Sigara Chang'ombe jijini Dar es Salaam walianza kushuhudia kazi ya kwanza ya mpiga solo mpya wa bendi ya Mlimani Park Adolf Mbinga.
                          
Mbinga aliyejiunga na bendi hiyo akitokea bendi mbalimbali zikiwemo African Stars 'Twanga Pepeta' Mchinga Sound na nyingine kadhaa alianza kuonyesha uwezo wake katika wimbo wa kwanza aliopiga na bendi hiyo unaoitwa 'Kukatika kwa Kidole Gumba'
Katika wimbo huo uliotungwa na Hassan Reheni Bitchuka, Mbinga alionyesha uwezo mkubwa katika ukung'utaji wa gitaa la solo.
Akizungumza katika onyesho hilo, Mbinga alieleza kuridhishwa kwake kuwepo kwenye bendi hiyo yenye wanamuziiki wenye uwezo na vilevile wanaojua jinsi ya kuishi na wenzao.
Alisema anakusudia kushiriki zaidi mkakati wa kuirudisha bendi hiyo kwa wapenzi wake katika siku chache zijazo.

No comments:

Post a Comment