STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, May 1, 2013

Azam waendelea kujiwinda Morocco

Kocha Stewart Hall akiwanoa wachezaji wake Morocco


WAWAKILISHI pekee wa Tanzania katika michuano ya kimataifa, Azam ambayo iko jijini Rabat kwa ajili ya mechi ya marudiano ya raundi ya pili ya Kombe la Shirikisho dhidi ya AS FAR Rabati ya huko inaendelea vizuri na mazoezi.

Kwa mujibu wa Ofisa Habari Msaidizi wa Azam FC, Jaffer Idd maandalizi yanakwenda vizuri kwa ajili ya mechi hiyo itakayochezwa Jumamosi (Mei 4 mwaka huu).

Msemaji huyo alisema wachezaji wana ari kubwa ya kuwapa raha watanzania na kuomba wazidi kuimbea kila la heri ili kupata ushindi Jumamosi na kutinga hatua ya 16 Bora ya michuano hiyo ya pili kwa ukubwa Afrika.

No comments:

Post a Comment