STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, May 1, 2013

Coastal yaibana Yanga, Lyon byebye VPL

Yanga iliyobanwa uwanja wa Taifa

maafande wa JKT Oljoro waliolazikisha suluhu kwa Ruvu Shooting

Coastal waliochelewesha sherehe za ubingwa za Yanga

Afican Lyon iliyoshuka rasmi Ligi Kuu baada ya kunyukwa na Mtibwa Sugar Manungu
WAKATI Mabingwa wapya wa Ligi Kuu Tanzania Bara Yanga wakishikwa kwenye uwanja wa Taifa na Coastal Union ya Tanga kwa kulazimishwa sare ya bao 1-1, African Lyon imezama rasmi Ligi Daraja la Kwanza baada ya kulazwa mabao 2-0 na Mtibwa Sugar.
Yanga ambayo inakamilisha tu ratiba ya ligi hiyo baada ya Ijumaa iliyopita kutawazwa mabingwa baadaya Azam kung'ang'aniwa na Coastal na kyutoka sare ya 1-1, ndiyo iliyokuwa ya kwanza kupata bao kupitia Jerry Tegete kabla ya Coastal kusawazisha dakika chache baadaye kupitia kwa Abdi Banda na kuzifanya timu hizo ziende mapumziko zikiwa nguvu sawa hali iliyoendelea hadi dakika 90 zilipoisha na hivyo kugawana pointi moja moja na Yanga kufikisha pointi 57 na Coastal 35.
Katika mechi nyingine iliyochezwa uwanja wa Chamazi, JKT Ruvu walijikuta wakizama kwa kulazwa mabao 2-1 na Prisons ya Mbeya, huku uiwanja wa Mabatini Mlandizi wenyeji Ruvu Shooting walibanwa na JKT Oljoro kwa kutofungana.
African Lyon inayoburuza mkia ilijihakikishia kucheza Ligi Daraja la Kwanza msimu ujao kwa kutunguliwa mabao 2-0 na Mtibwa Sugar katika pambano jingine lililochezwa uwanja wa Manungu, mjini Turiani. Mabao yoye ya washindi yakiwekwa kimiani na mshambuliaji nyota Hussein Javu katika dakika ya 30 na 59.
Mechi nyingine ya ligi hiyo ilichezwa mjini Morogoro kati ya Polisi Moro dhidi ya wageni wao Kagera Sugar iliyoisha kwa wenyeji kushinda bao 1-0 na kuifanya timu hiyo kuendelea kuvuta pumzi kusubiri kuona hatma yao katika ligi hiyo kwa kufikisha pointi 22 sawa na Toto African..

No comments:

Post a Comment