STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, May 18, 2013

Mbunge Chadema aanguka ghafla Bungeni


Mhe. Taratibu Abama
MBUNGE wa Viti Maalum, pichani Mwanamrisho Taratibu Abama (Chadema), ameanguka  bungeni, baada ya kujisikia vibaya.

Mbunge huyo alianza kujisikia vibaya, hali iliyomfanya kuketi katika viti vilivyo karibu na zahanati ya Bunge.
Kwa mujibu wa watu walioshuhudia walisema mbunge huyo alipata huduma ya kwanza katika zahanati hiyo kwa zaidi ya saa mbili kabla ya kupelekwa katika Hospitali ya  Rufaa ya Mkoa ya Dodoma.Kwa mujibu wa taarifa kutoka ndani ya hospitali hiyo, zinasema mbunge huyo alilazwa wodi namba 18.

Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma, Dk. Zainab Chaula, alithibitisha kupokelewa kwa mbunge huyo.
“Ni kweli yupo hapa  na hali yake inaendelea vizuri sasa ,”alisema.

No comments:

Post a Comment