STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, May 22, 2013

Msouth kuzihukumu Stars na Morocco, TFF yaanika ratiba ya mazoezi ya Stars


https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj5ta_2ly1qlzIPEMvk9-7RZw-jUtAQOF_M1x8hzY9FkGokWUR35u8p492S6fv93ojEEaSwnv5Isx0Oqz1sXA0ns71kzAKekOc-WhQCB9ETEs3ExFRGtjo1Zz6_8tQNl1uqOcAqy2IGfwjF/s1600/Daniel_Bennett.jpg
Refa Frasser Daniel Bennett atakayezichezesha Tanzania na Morocco

Na Boniface Wambura
SHIRIKISHO la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) limemteua mwamuzi kutoka Afrika Kusini kuchezesha mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia, Kanda ya Afrika kati ya Tanzania (Taifa Stars) na wenyeji Morocco (Lions of the Atlas).

Mechi hiyo ya kundi C itachezwa Juni 8 mwaka huu jijini Marrakech, Morocco kwenye Uwanja wa Grand kuanzia saa 3 kamili usiku kwa saa za Morocco. Mwamuzi atakayechezesha mechi hiyo ni Fraser Daniel Bennett.

Bennett atasaidiwa na Thusi Zakhele Siwela pia wa Afrika Kusini, wakati mwamuzi msaidizi namba mbili atakuwa ni Marwa Range kutoka Kenya. Mwamuzi wa akiba (fourth official) ni Lwandile Mfiki wa Afrika Kusini.

Kamishna wa mechi hiyo ni Robert Mangollo-M’voulou wa Gabon wakati mtathimini wa waamuzi (referee assessor) ni Charles Masembe kutoka Uganda.

Taifa Stars ambayo iko chini ya Kocha Kim Poulsen, na ikidhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager tayari iko kambini katika hoteli ya Tansoma ikiendelea kujinoa kwa ajili ya mechi hiyo ambapo kabla itajipima na Sudan (Nile Crocodiles) Juni 2 mwaka huu jijini Addis Ababa, Ethiopia.



Ratiba ya mazoezi kwa timu hiyo ni kama ifuatavyo;
Mei 22                 Saa 10 jioni                             Uwanja wa Karume

Mei 23                 Saa 1 asubuhi na Saa 10 jioni   Uwanja wa Karume

Mei 23                 Saa 10 jioni                             Uwanja wa Karume

Mei 25                 Saa 1 asubuhi na Saa 10 jioni     Uwanja wa Karume

Mei 26                 Saa 3 asubuhi                            Uwanja wa Karume


No comments:

Post a Comment