STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, May 22, 2013

Pellegrini athibitika kuondoka Malaga, milango i wazi kutua Man City

http://images.gazzetta.it/Media/Foto/2009/10/30/pelle_01.JPG
Kocha Manuel Pellegrini

MENEJA wa timu ya soka ya Malaga ya Hispania, Manuel Pellegrini amethibitisha kuwa ataondoka katika klabu hiyo mwishoni mwa msimu wa Ligi Kuu ya nchi hiyo.
Duru za michezo zinasema kuwa, Pellegrini atajiunga na Manchester City kuchukua nafasi ya kocha aliyetimuliwa katika timu hiyo, Muitaliano Roberto Mancini.
Kocha huyo alithibitisha mapema leo kwamba ataondoka katika benchi la ufundi la timu hiyo aliyokuwa akiinoa tangu mwaka 2010.
Akinukuliwa na mtandao wa Marca.com wa gazeti moja la nchini humo , kocha huyo alisema yeye na klabu hiyo wanaelekea kuachana, lakini umoja wao utaendelea kuwepo hata kama watatenganishwa na miji watakayokuwepo.
"Naondoka," alinukuliwa kocha huyo aliyoifikisha Malaga kwenye Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya kabla ya kutolewa na  Borussia Dortmund ambayo inatarajiwa kuvaana na wapinzani wao wa Ujerumani, Bayern Munich siku ya Jumamosi katika pambano la Fainali za mwaka huu.

No comments:

Post a Comment