STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, May 29, 2013

Yathibitika M2P hajafa, ila bado yu mahututi

ASUBUHI zilizagaa taarifa nchini kwamba msanii aliyekuwa na marehemu Albert Mangwea 'Ngweair', M to the P aliyekutwa amezimia kwamba naye alikuwa amefariki dunia, ukweli ni kwamba msanii huyo bado yu hai ingawa hali yake inaelezwa kuwa bado si nzuri kwani anaendelea kupumulia gesi.
Kwa mujibu wa Mtangazaji wa kituo cha radio cha Clouds Fm, Millard Ayo, aliyekuwa akizungumza moja kwa moja kutoka Afrika Kusini alipoenda, alisema kuwa M2P bado yu hai, ingawa bado amelazwa na anapumua kwa kutumia mashine maalum.
Ayo alisema M2P aliyekuwa sambamba na Ngweair katika chumba kimoja, alionekana na baadhi ya marafiki zake akiwamo msanii Bushoke akinyanyuka mara aalipowaona wameenda kumjulia hali na kuthibitisha kuwa yu hai tofauti na taarifa za mapema asubuhi kwamba msanii huyo naye aliaga dunia.
Aidha mtangazaji huyo anayeendesha kipindi cha Amplifaya, alisema mwili wa marehemu Ngweair ulihamishw atoka hospitali ya Helen Joseph na kupelekwa hospitali ya serikali ukisubiri taratibu za kuusafirisha kuurejesha Tanzania kwa ajili ya mazishi.

No comments:

Post a Comment