STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, June 17, 2013

LUCY CHARLES NDIYE KISURA WA JIJI LA MWANZA


SHINDANO la kumsaka mrembo wa mkoa wa Mwanza kwa mwaka 2013, kiliteguliwa mwishoni mwa wiki iliyopita baada ya Lucy Charles, msomi wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustino kuwabwaga warembo wengine 13 waliojitokeza kuwania taji hilo.

Nyota ya mrembo huyo ilianza kuonekana mapema katika mavazi yote aliyovaa, lakini zaidi aliwapagawisha mashabiki wa urembo waliofurika katika ukumbi wa Yatch club baada ya kujibu swali kwa ustadi lililouliza ni changamoto ipi kubwa walionayo vijana wa leo.

Mshindi wa pili katika shindano hilo alikuwa Judith Josephat na mshindi wa tatu ni Suzan Ikombe.
Washindi hao watauwakilisha mkoa wa Mwanza katika shindano la kanda ya ziwa litakalofanyika mwishoni mwa mwezi huu.

No comments:

Post a Comment