STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, July 30, 2013

Lionel Mess awafunika, Ribery, Ronaldo tuzo za Goal 50



 http://www.goolfm.net/wp-content/uploads/2013/07/messi-goal-50.jpg
MADRID, Hispania
LIONEL Messi ameshinda Tuzo ya Mwanasoka Bora wa Dunia ya ‘Goal 50’ inayotolewa na tovuti maarufu ya soka duniani ya goal.com baada ya kumaliza msimu mwingine huku akiandika rekodi mpya.
Mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Argentina alitwaa tuzo hiyo kwa mara ya tatu baada ya kuandika rekodi ya mabao katika msimu ambao alivunja rekodi ya Gerd Muller iliyodumu kwa miaka 40 ya kufunga magoli 85 katika mwaka wa kalenda.
Messi mwenye miaka 26, alifunga magoli 91 mwaka wa 2012 na kuongeza jumla ya mabao yake akiwa ndiye mfungaji kinara mwenye mabao mengi zaidi katika historia ya Barcelona baada ya kufikisha magoli 313 katika michuano yote kufikia mwisho wa msimu uliopita.
Messi alifunga katika mechi ya 19 mfululizo kwenye mechi za La Liga, Ligi Kuu ya Hispania Machi 2013, hivyo kuwa mwanasoka wa kwanza katika historia kufunga mfululizo dhidi ya wapinzani wao wote katika ligi kuu ya soka la kulipwa.
Baada ya kupokea tuzo yake kutoka kwa mwakilishi wa Goal mjini Barcelona, Pilar Suarez, wakiwa kwenye uwanja wa mazoezi wa timu hiyo, Messi alisema: "Nimevutiwa sana na tuzo. Kama wachezaji, tunafanya kazi mwaka mzima ili kutwaa mataji kwa ajili ya timu, hatutafuti tuzo binafsi, lakini wakati zinapokuja huwa zinatutia moyo na kutuongezea nguvu ya kuendeleza kiwango."
Tuzo ya ‘Goal 50’ inachukuliwa kuwa moja ya tuzo zinazoheshimiwa sana katika michezo kwa sababu uteuzi wake hufanywa na tovuti kubwa zaidi ya soka duniani.
Kura hupigwa mwishoni mwa msimu wa ligi za nyumbani za nchi nyingi duniani na pia wa mechi za kimataifa.
Zaidi ya waandishi 500 wa tovuti ya Goal kutoka maeneo mbalimbali duniani hupiga kura kuchagua nyota 50-bora, hivyo kutoa nafasi kwa wachezaji wengi zaidi.
Messi ameibuka kinara wa orodha ya mwaka huu dhidi ya Franck Ribery aliyemaliza katika nafasi ya pili baada ya kuisaidia Bayern Munich kutwaa mataji matatu msimu uliopita likiwamo la Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya. Mshindi wa mwaka jana, Cristiano Ronaldo ametwaa nafasi ya tatu.

WASHINDI WOTE TUZO ‘GOAL 50’
2008     Cristiano Ronaldo
2009     Lionel Messi
2010     Wesley Sneijder
2011     Lionel Messi
2012     Cristiano Ronaldo
2013     Lionel Messi
----------

No comments:

Post a Comment