STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, August 13, 2013

Haya ndiyo majina ya wanaodaiwa wauza Unga na Bangi nchini



Majina ya watanzania 255 wanaojihusisha na biashara ya dawa za kulevya   yamejulikana  na  JAMHURI  imeamua kuyachapisha...
 
Uchunguzi uliofanywa umebaini kuwa kwenye orodha hiyo wapo watu maarufu na baadhi wamekuwa wakitoa misaada ,huku wengine wakijifanya ni wazee  wa kanisa na kushiriki  shughuli mbalimbali za kijamii....
 
Uchunguzi wetu usio na chembe ya shaka  unaonesha kuwa orodha hii ya watu watakaoandikwa hapo chini kwa sasa wapo chini ya uangalizi wa mahakama na polisi..
 
"Ni kweli kuna watu tumewapeleka mahakamani, huko wamewekwa chini ya uangalizi na wanatakiwa kuripoti  kwa  muda wanaopangiwa.Tunafanya hivyo baada ya uchunguzi wetu kubaini kwa ni kweli  wanahusika na biashara hii haramu."Alisema  Nzowa
Nzowa aligoma kuyataja majina hayo, lakini uchunguzi uliofanywa na JAMHURI  kutoka ndani ya jeshi la polisi na  mahakama  umefanikiwa  kuyapata  majina  hayo...
Katika orodha hii, yumo mchungaji aliwekwa chini ya uangalizi , na baada ya kumaliza muda huo, siku tatu baadaye alikamatwa na  dawa nchini Brazil.Pia yumo Sheikh anayetoa misaada mbalimbali,lakini baada ya kukamatwa na dawa kilo 211, eneo la Kunduchi Dar es salaam, kwa sasa  amekimbilia  Afrika kusini....
DAWA ZINAVYOINGIZWA NCHINI:
Hadi sasa kiwango kikubwa cha dawa za kulevya kinaingizwa nchini kwa njia ya meli katika bahari ya Hindi.
Baada ya meli kuwasili Tanzania, wasafirishaji hutumia boti ndogo ziendazo kasi kuchukua dawa hizo.Maeneo yanayotumiwa zaidi kuingiza dawa ni Bagamoyo, Zanzibar, Tanga na Mtwara....
Jijini Dar, boti hizo hutia nanga  katika eneo la  Bagamoyo ambako pia ndiko kwenye njia kuu ya uingizaji  wa bidhaa za magendo  zisizolipiwa kodi...
Biashara  hiyo  haramu  huwahusisha  baadhi  ya  polisi  ambao  mara  kadhaa  wamekuwa  wakiwapa  ulinzi   wahalifu  hao.
Viwanja  vya  ndege   vinavyotumiwa  kuingiza  madawa  ya  kulevya  ni  Julius  Nyerere ( DAR )  na  Abeid  Amani  Karume ( ZANZIBAR)
Taarifa  toka  kitengo  cha  kuzuia  dawa  za  kulevya   zinasema  kuwa  wasafirisha  wanaotumia  ndege  wamekuwa  wakibuni  mbinu  mbali  mbali  zikiwemo  za  kutumia  manukato  kwa  ajili  ya  kuwapumbaza mbwa  wenye  mafunzo  ya  kubaini  madawa  ya  kulevya....
Habari zaidi  zinasema  kuwa  kitengo  kimepata  vifaa  maalumu    vya  kubaini  kama  ndani  ya  mizigo  kuna  madawa  ya  kulevya. Vifaa  hivyo  ni  mfano  wa  sindano  ambayo  huchomwa  kwenye  mizigo  na  kuipitisha  kwenye  ngozi  ya  mwili.
Kama  kuna  dawa, ikigusishwa  kwenye  ngozi  unga  hupukutika  na  kama  mzigo  hauna  dawa  za  kulevya  basi  hakuna  kitakachotokea....
Tayari  vifaa  hivyo  vimeanza  kutumika  katika  uwanja  wa  kimataifa wa  Julius  Nyerere.
Lisake gazeti la Jamhuri utaiona orodha nzima ya majina hayo 250.
 
Source: Gazeti la Jamhuri.

No comments:

Post a Comment