STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, August 3, 2013

NMB yatoa msaada wa mashuka Hospitali ChakeChake Pemba


 Meneja wa Tawi la Benki ya NMB Chake Chake, Pemba, Hamidu Mughamba, (kulia) akimkabidhi Katibu Tawala wa Mkoa, Mhe. Hanuna Ibrahim, sehemu ya mashuka yaliyotolewa na Benki hiyo kama msaaada kwa hospitali za Wilaya ya Chake Chake.
 
NMB imekuwa mstari wa mbele katika kuchangia mahitaji mbalimbali yanayoizunguka jamii.Kwa kutambua hilo hivi karibuni  maofisa wa NMB tawi la Chake chake walitoa mashuka ya hospitali yenye thamani ya shilingi million tano kwenye hospitali mbali mbali ikiwamo hospitali ya wilaya ya Wete, Chakechake, Mkoani na Micheweni. Mashuka haya  yatasaidia kupunguza hitaji kubwa la mashuka lililokua likizikumba hospitali hizi.

 Maofisa wa Benki ya NMB pamoja na Mganga Mkuu wa Hosipitali ya Chake Chake, Pemba, wakiyatizama baadhi ya mashuka  yaliyokabidhiwa na Benki ya NMB.
Maofisa wa Benki ya NMB pamoja na Mganga Mkuu wa Hosipitali ya Chake Chake, Pemba, wakiyatizama baadhi ya mashuka  yaliyokabidhiwa na Benki ya NMB.

No comments:

Post a Comment