STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, August 3, 2013

Hamis Kiiza mshambuliaji wa 7 Jangwani

MSAHAMBULIAJI WA YANGA HAMIS KIIZA ASAINI MKATABA WA MIAKA MIWILI KUENDELEA KUKIPIGA YANGA

MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Uganda, Hamis Kiiza hatimaye amesaini mkataba wa miaka miwili kuendelea kuitumikia klabu hiyo ya Jangwani na kufanya idadi ya washambuliaji katika kikosi hicho cha Jangwani kufikia saba mpaka sasa. 
Kiiza alisaini mkataba huo katika hoteli ya Protea, Dar es Salaam na kufanya idadi ya wachezaji wa kimataifa kufikia wanne akiwamo Haruna Niyonzima wa Rwanda, Mbuyu Twitte wa DR Congo na Didier Kavumbagu kutoka Burundi.

Kusainishwa kwa Mganda huo kumemaliza sintofahamu ya muda mrefu juu ya mustakabali wa mchezaji huyo aliyeibeba Yanga tangu alipotua klabuni hapo na kufanya safu ya mbele ya jangwani iwe na wafumania nyavu saba.
 
Wakali wengine ni Jerryson Tegete, Kavumbagu, Hussein Javu, Said Bahanuzi Shaban Kondo (aliyesajiliwa toka Msumbiji) na Realintus Lusajo (kutoka Machava- Moshi).

No comments:

Post a Comment