STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, August 27, 2013

Timu za Ruvu zachekelea kuanza vyema, yapania wapinzani wao wa Mbeya

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhaF1tsqvUmrtMICozA4dHcA_DetF8axYj97O_uDj0kkxxGOF6_BpM4UZbrAuxFzz8p04g6_20F6Y4D6lFqVkIPGh9tQ3Ad3NlFKR5UQCPex36z5AyqjybyV9U-_8S_GqOtYG6DPFj3-2QH/s640/JKT+RUVU+KIKOSI.jpg
JKT Ruvu
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhXtdUgJUQpoqJDsDusQZKcGKBjAz5VsgkU1d7LoYMp8k9R4EJMliB6GKtLSqbJpXRRbSWfurfjs0QQYhasY-3DPyM87v27C4nM5jOY7vrLhH7s7iM01OrbSAtJ0p-IIcVEFh_2tSEaTI4E/s640/RUVU+SHOOTING.jpg
Ruvu Shooting
UONGOZI wa timu za Ruvu Shooting na JKT Ruvu za Pwani umefurahishwa na kuwapongeza makocha na wachezaji wao kwa kuanza vyema msimu mpya wa Ligi Kuu Tanzania Bara kwa kupata ushindi wakidai huo ni mwanzo tu.
Ruvu Shooting ilianza kwa kishindo ligi hiyo kwa kuinyuka Prisons ya Mbeya kwa mabao 3-0,  wakati maafande wenzake wa JKT walipata ushindi wa 2-0 jijini Tanga walipoumana na Mgambo JKT.
Ushindi huo umeziweka timu hizo kileleni sambamba na Yanga walioishindilia Ashanti United kwa mabao 5-1 katika mechi za ufunguzi wa ligi hiyo mwishoni mwa wiki na kuufanya uongozi wa klabu hizo kuwapongeza kwa kazi nzuri.
Afisa Habari wa timu hizo za JKT, Masau Bwire alisema uongozi unawapongeza makocha Charles Boniface na Mbwana Makatta na wasaidizi wao pamoja na wachezaji wa kuanza vyema pazia la ligi kuu kwa kupata ushindi.
"Tumefurahishwa na mwanzo nzuri uliofanywa na timu zetu na tunawapongeza makocha na wachezaji kwa kazi nzuri waliyofanya tukiamini wataendelea kugawa dozi hata katika mechi zijazo. Hii ni tahadhari kwa wapinzani wetu msimu huu," alisema Bwire.
Bwire alisema kwa sasa timu zao zinaelekeza nguvu kwa mechi zao za kesho ambapo Ruvu Shooting itakuwa ugenini mjini Mbeya kuumana na Mbeya City, wakati 'ndugu' zao JKT Ruvu watakuwa Mabatini, Mlandizi kuvaana na Prisons.

No comments:

Post a Comment