STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, August 27, 2013

Mpinzani wa Cheka kutua leo, Mashali bado 'amgomea' Maugo

http://www.minnesotaboxing.com/Interviews/phil_codrington.jpg
Bondia Phil 'The Drill'  Williams
Phil "The Drill" Williams/ SnapLocally.com
Phil 'The Drill' Williams
WAKATI bondia Phil 'The Drill' Williams kutoka Marekani pamoja na kocha na daktari wake wanatarajia kutua nchini usiku wa leo ili kumkabili Francis Cheka, Thomas Mashali ameendelea kusisitiza kuwa hatapigana na Mada Maugo siku ya Ijumaa.
Cheka na Williams wanatarajiwa kupigana kuwania ubingwa wa kimataifa wa WBF katika pambano la uzani wa Super Middle raundi 12 kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee, jijini Dar es Salaam siku ya Agosti 30.
Rais wa TPBO-Limired wanaosimamia pambano hilo na mingine itakayochezwa siku hiyo, Yasin Abdallah 'Ustaadh' alisema usiku wa jana wametuma tiketi ya bondia huyo na wasaidizi wake na watatua nchini leo saa nne kasorobo usiku.
Ustaadh alisema Mmarekani kutua kwa bondia huyo ni kuonyesha maandalizi ya pambano hilo yamepamba moto huku akiwaonya mashabiki na mabondia wasio na nidhamu kujihadhari mapema siku ya pambano kwa ulinzi utakaokuwepo.
"Bondia wa Marekani Phil Williams atatua nchini Saa 3:50 usiku wa kesho (leo) akiwa na kocha wake, Filbert Songola na Dk aitwaye Charles na TPBO-Limited tunawaonya mashabiki kujiepusha na uhuni siku ya pambano," alisema.
Alisema onyo hilo wanalitoa mapema kutokana na ukweli mapambano hayo yanatarajiwa kuhudhuriwa na mabalozi, mawaziri na viongozi wenye heshima zao na kwamba ulinzi utakuwa mkali hiyo asingependa wachache kuwavurugia.
Katika hatua nyingine bondia Thomas Mashali ameendelea kusisitiza kuwa hatapanda ulingoni Ijumaa kuzipiga na Mada Maugo akisema halitambui pambano hilo.
"Msimamo wangu ni ule ule kwa sasa akili yangu ipo kwenye pambano la kimataifa dhidi ya Mmalawi Chiotcha Chimwemwe nitakayepigana naye mjini Blantire nchini Malawi," alisema Mashali maarufu kama Simba  Asiyefugika.
Mashali alisema wameingia mkataba wa kupigana na Chimwemwe katika pambano la uzito wa kati litakalochezwa Oktoba 29 na kudai kwa kutambua ukali wa mpinzani wake ameanza mapema kujifua ili aweze kufanya vyema.

No comments:

Post a Comment