STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, September 23, 2013

Yathibitishwa Mtanzania ajeruhiwa tukio la ugaidi Kenya

36
WIZARA ya Mambo ya Nchi za Nje ya Tanzania imesema kuwa hadi kufikia leo Septemba 23, 2013 ni Mtanzania mmoja tu aliyetambulika kwa jina la Bwana Vedastus Nsanzugwanko mwenye cheo cha Umeneja katika kitengo cha Ulinzi wa Watoto, cha Shirika la Umoja wa Mataifa la Hazina ya Kuhudumia Watoto (Child Protection, UNICEF) ambaye taarifa zake ziliifikia Ofisi ya Balozi kuwa amejeruhiwa kwa risasai na milipuko ya maguruneti kwenye miguu yake yote miwili.

Taarifa hiyo inasema kuwa kwa sasa hali Bwana Vedastus inaendelea vizuri akiwa anapatiwa matibabu alikolazwa katika hospitali ya Aga Khan ya jijini Nairobi, Kenya.

Imetaarifiwa kuwa Ubalozi unaendelea kufuatilia kwa lengo la kupata taarifa zaidi endapo kutakuwepo Watanzania wengine waliodhurika katika tukio hilo.

Ofisi ya Ubalozi kwa kushirikiana na Uongozi wa Chama cha Watanzania nchini Kenya (TWA) unaandaa utaratibu maalumu utakaowezesha TWA kuitikia wito uliuotolewa wa kuchangia damu kwa ajili ya kuwasaidia wahanga.


Chanzo: Taarifa ya Wizara ya Mambo ya Nje

No comments:

Post a Comment