STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, October 9, 2013

Mfanyabiashara mwingine amwagiwa Tindikali, safari hii Arusha

 
MFANYABIASHARA mkazi wa Sakina jijini Arusha, Japhet Minja anadaiwa kumwagiwa kitu kinachosadikiwa kuwa ni tindikali na watu wasiofahamika na kuachwa na majeraha usoni na mikononi.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka Arusha zinasema kuwa Minja alikumbwa na tukio hilo eneo la Shamsi Kata ya Elarai baada ya kumwagiwa kimiminika hicho na kuachwa na maumivu makali.
Akizungumza katika hospital ya Seriani alikola wa, Minja ambae ni mfanyabiashara adai alisimamishwa na watu waliomtaka kuongozana nao kwa ajili ya masuala ya kibiashara na ghafla wakiwa njiani ghafla alizuiwa na watu hao waliofunga njia na kumdhuru.
Daktari wa zamu aliyempokea mgonjwa huyo Godbless Masawe amesema walimpokea
mgonjwa huyo jana asubuhi akiwa na fahamu lakini baadae hali ilibadilika na
kulazimika kumpeleka katika chumba cha wagonjwa mahututi na kwa sasa Minja anaendela vyema kwa sasa.

No comments:

Post a Comment