STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, November 18, 2013

Nsajigwa amfagilia Samatta tuzo za Afrika

Shadrack Nsajigwa
Mbwana Samatta
NAHODHA wa zamani wa Yanga na Taifa Stars, Shadrack Nsajigwa, amewataka Watanzania kumuunga mkono Mshambuliaji wa Kimataifa wa Tanzania, Mbwana Samatta baada ya nyota huyo kuteuliwa miongoni mwa wachezaji 25 wanaocheza soka barani Afrika kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa Mwaka.
Nsajigwa alisema watanzania wanapaswa kumuombea Mungu Samatta ili kuweza kufanya vyema katika tuzo hizo akidai kuwa mchezaji huyo ni mkubwa kwa sasa na alistahili kufika hapo alipofikia.
Katika ujumbe wake kupirtia mtandao wa Facebook, Nsajigwa alisema hakuna maana yoyote kwa watanzania kumbeza Samatta kama walivyokuwa wakifanya kupitia maoni yao katika mtandao huo kwa madai huko ni kukojikubali vyetu ilihali Samatta amewatoa kimasomaso Watanzania kiasi cha kutakiwa kumfurahia kwa mafanikio yake.
Janani Watanzania wenzangu wapenda mpira, hatuna budi kumpa sapoti na kumuombea mchezaji wetu kuliko kumbeza, tuache mambo ya kishabiki hayatufikishi kokote. Kwa sasa Samatta ni mchezaji mkubwa na anastahili kuwa pale. Ahsanteni," ujumbe wa Nsajigwa uliosomeka hivyo.
Samatta anayeichezea klabu ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Watu wa Kongo, alitangazwa na Shirikisho la Sokla Afrika (CAF) kuwea miongoni mwa wachezaji wanaowania tuzo ya wachezaji wa klabu za ndani akiwa ni mmoja wa wachezaji wawili pekee wa kuanda wa Afrika Mashariki kuteuliwa katika tuzo za Afrika zitakazotolewa mwakani,. Mwingine ni Mkenya Victor Wanyama wa Kenya anayewania Tuzo ya Mwanasoka Bora wa Afrika-2013.
Nyota huyo wa zamani wa African Lyon na Simba amekuwa mhimili mkubwa wa timu ya TP Mazembe akitajwa kama kipenzi cha mashabiki wa klabu hiyo ya Kongo ambayo ipo katika Fainali za Kombe la Shirikisho, nyuma ya Tresor Mputu.
Orodha kamili ya wanaowania tuzo za Mwanasoka Bora wa klabu za ndani ya Afrika ambapo Samatta yumo ni kama ifuatavyo;
1. Adane Girma - Ethiopia - St George
2.Ahmed Fathi - Egypt - Al Ahly
3. Alexis Yougouda Kada - Cameroon - Coton Sport
4. Ali Machani - Tunisia - CAB
5. Bapidi Fils Jean Jules - Cameroon - Coton Sport
6. Daine Marcelle-Klate - South Africa - Orlando Pirates
7. Fakhreddine Ben Youssef - Tunisia - CSS
8. Getaneh Kebede - Ethiopia - Bidvest Wits
9. Idrissa Kouyate - Cote d'Ivoire - CS Sfaxien
10. Iheb Msakni - Tunisia - Esperance
11. Luyanda Lennox Bacela - South Africa - Orlando Pirates
12. Mbwana Samatta - Tanzania - TP Mazembe
Mbwana Samatta
13. Moez Ben Cherifia - Tunisia - EST
14. Mohamed Aboutrika - Egypt - Ahly
15. Rainford Kalaba - Zambia - TP Mazembe
16. Senzo Meyiwa - South Africa - Orlando Pirates
17. Soumbeila Diakite - Mali - Stade Malien
18. Sunday Mba - Nigeria - Warri Wolves
19. Tresor Mputu - DR Congo - TP Mazembe
20. Waleed Soliman - Egypt - Al Ahly
21. Yannick N'djeng - Cameroon - EST

Mwisho

No comments:

Post a Comment