STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, November 18, 2013

Golden Bush Veterani yawanyoa wazee wenzao

Kikosi cha Golden Bush Veterani
Benchi la ufundi la timu hiyo
WAKALI wa kandanda kwa timu za maveterani jijini Dar er Salaam, Golden Bush juzi iliwanyoa wazee wenzao wa Kivukon Veterani kwa mabao 3-0 kablka ya jana kupata ushindi mwingine dhidi ya Kijitonyama.
Ushindi wa juzi dhidi ya Kivukoni ulikuwa ni wa kulipa kiasi kwa wakali hao ambao wiki chache za nyuma walifumuliwa na wapinzani wao hao.
Golden Bush ilipata ushindi huo katika uwanja wa Kinesi Ubungo kwa mabao yaliyowekwa kimiani na Abuu Ntiro, Said Sued 'Panucci' na Mgaza Aguero.
Mlezi wa klabu hiyo yenye maskani yake Sinza, Onesmo Waziri 'Ticotico' alisema ushindi huo mfululizo kwa timu yake umewapa faraja.
Ticotico alisema kwa sasa kikosi chao kinajiandaa kwa ajili ya ziara ya kwenda visiwani Zanzibar kuvaana na wazee wa huko katika mehci ya kuadhimisha siku ya Uhuru, Desemba 9.

No comments:

Post a Comment