STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, November 20, 2013

Ufaransa, Ugiriki, Croatia nao hizooo Brazili 2014

Benzema na wenzake wakishingilia bao alililofunga katika mechi yao ya usiku wa jana
MABINGWA wa Dunia wa mwaka 1998, Ufaransa jana walifanikiwa kufuzu kimiujiza mbele ya Ukraine kwenda kwenye Fainali za mwakani za Kombe la Dunia baada ya kupata ushindi mnono nyumbani wa mabao 3-0.
Ufaransa walionyukwa mabao 2-00 na wapinzani wao ugenini wiki iliyopita ilipata ushindi huo usiku wa jana na kufuzu kwa jumla ya mabao 3-2.
Mabao ya Mamadou Sakho, Karim Benzema na lile la kujifunga la Oleh Husyev iliisaidia Ufaransa kuungana na timu za Ureno, Ugiriki na Croatia kupenya katika kapu kushiriki fainali hizo za Dunia zitakazoifanyika nchini Ufaransa.
Kipigo cha awali cha mabao 2-0 kilikuwa kikiitisha Ufaransa kuzikosa fainali hizo, lakini Sakho aliianza kupunguza magoli kwa kufunga bao la kwanza dakika ya 22 kabla ya Benzema kuongeza jingine dakika ya 34. 
Kipindi cha pili mchezaji wa Ukraine katika harakati za kuokoa bao alijikuta akiiusindikiza wavuni katika dakika ya 72 na kupa tiketi Ufaransa bila kutegemewa na wengi.

No comments:

Post a Comment