STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, November 20, 2013

Ghana, Algeria kafuzu Fainali za Kombe la Dunia 2014

Algeria na Burkina Faso zilipokuwa zikiumana
TIMU za taifa ya Ghana na Algeria zimekata tiketi za kucheza Fainali za Kombe la Dunia 2014 zitakazofanyika nchini Brazil baada ya kupata matokeo tofauti katika mechi zao za mkondo wa pili za hatua ya mtoano.
Algeria ikiwa nyumbani ikiisimamisha Burkina Faso kwa kuilaza bao 1-0 lililokuwa likihitajika, huku Ghana wakichezeea kipigo cha mabao 2-1, lakini ikifuzu kutokana na ushindi mnono wa mabao 6-1 iliyopata katika mechi ya mkondo wa kwanza dhidi ya Misri.
Waalgeria walipata bao hilo mapema kipindi cha pili, kupitia kwa Madjid Bougherra na kufanya matokeo ya jumla yawe 3-3, baada ya awali Burkina Faso kushinda mabao 3-2.
Ghana wakiwa na hazina kubwa ya ushindi ilipigana kiume mbele ya wenyeji wao Misri walipata mabao mawili ya kila kipindi kutoka kwa Amri Zakhy na Gedo kabla ya Kelvin Prince Boateng kufunga bao la kufutia machozi dakika za 'jioni' akitokea benchi.
Algeria na Ghana sasa zinaungana na Cameroon, Ivory Coast, na Nigeria kukamilisha idadi ya timu tano za Afrika kwenda Brazil mwakani.

No comments:

Post a Comment