STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, November 16, 2013

Ureno yaichinja Sweden, Ugiriki yanusa Brazil, Ufaransa Mmh!

http://news.bbcimg.co.uk/media/images/71150000/jpg/_71150286_71150285.jpg
Ronaldo akipongezwa baada ya kuifungia Ureno baoa pekee jana dhidi ya Sweden
Clash of the titans: Portugal's Cristiano Ronaldo (left) and Sweden's Zlatan Ibrahimovic shake hands before kick off
Ronaldo na Ibrahimovic walipokuwa wakilisimiana kabla ya pambano, wote ni manahodha wa nchi zao
CRISTIANO Ronaldo amethibitisha yeye ni bora kuliko Zlatan Ibrahimovic baada ya usiku wa jana kuiongoza Ureno kupata ushindi kiduchu nyumbani kwao dhidi ya Sweden katika pambano la mkondo wa kwanza wa mtoano wa kuwania kutinga Fainali za Kombe la Dunia kwa timu za Ulaya.
Pambano la pambano la timu hizo mbili, lakini pia kulikuwa na maneno ya chini chini kuwapambanisha wakali hao wawili na Ronaldo alionyesha anaweza kumzima Ibrahimovic anayecheza PSG kwa kufunga bao pekee lililoipa ushindi Ureno, japo bado nchi hiyo haina uhakika wa kwenda Brazil mwakani.
Bao hiulo la Ronaldo alilifunga kwa kichwa dakika ya 82 kuunganisha krosi ya Miguel Veloso na kuifanya Ureno kusubiri matokeo ya mechi ya mkondo wa pili itakayochezwa mapema wiki ijayo ugenini dhidi ya wenyeji wao Sweden ambao wana rekodi nzuri kwenye dimba lao la nyumbani.
Katika mechi nyingine za 'kapu' Ukraine iliizima Ufaransa kwa mabao 2-0 na kujiweka kwenye nafasi nzuri ya kusonga mbele, huku Ugiriki ikiwa nyumbani ikaifyatua Romania mabao 3-1, huku Iclenad na Croatia zikitoshana nguvu kwa kwenda suluhu ya bila kufungana.
Mechi za mkondo wa pili zitakazoamua hatma ya wawakilishi wa mwisho wa Bara Ulaya zitachezwa siku ya Jumanne.

No comments:

Post a Comment