STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, January 3, 2014

Arsena majanga, Bendtner aongezeka wodi ya majeruhi Emirates

NICKLAS Bendtner anajiandaa kukaa nje ya uwanja kwa "wiki kadhaa" kutokana na majeraha ya 'enka' yanayowafanya vinara hao wa Ligi Ku ya England wakiwa na upungufu wa washambuliaji.
Mchezaji huyo wa kimataifa wa Denmark aliingia kutokea benchi na kufunga goli la kuongoza la Gunners katika ushindi wa 2-0 dhidi ya Cardiff lakini akaumia 'enka' wakati akifunga goli hilo.
Mfungaji anayeongoza Olivier Giroud alikosa mechi hiyo kutokana na majeraha ya 'enka' pia.
"Inaonyesha tumepungukiwa," alisema kocha Arsene Wenger, huku dirisha la usajili likifunguliwa.
Hata hivyo, kocha huyo hakutaka kubainisha kama anawania kusajili mshambuliaji mwezi huu, licha ya Bendtner kutarajiwa kuwa nje katika mechi ya kesho ya Kombe la FA nyumbani dhidi ya Tottenham, na Giroud akiwa shakani zaidi.
Wenger alisema: "Yeye (Bendtner) aliumia enka, kwa muda gani atakuwa nje hatujui lakini inaonekana ni wiki kadhaa.
"Tunaye Lukas Podolski na Theo Walcott ambao wanaweza kucheza kama washambuliaji wa kati lakini kwa mipango ya muda mrefu tunahitaji mtaalamu wa nafasi hiyo ya kati.
"Kwa kuwapoteza wachezaji wawili ni ngumu. Msiwe na haraka sana kwa sasa, tunachosema ni kwamba tuna washambuliaji wawili ambao ni majeruhi."
Kuhusu Bendtner, Wenger alisema anaonekana kurejea kucheza vile anavyotaka hivyo anapenda kuendelea kuwa naye, lakini hatamzuia akitaka kuondoka.
Arsenal pia iliwakosa Aaron Ramsey (paja), Mesut Ozil (bega), Kieran Gibbs (kiazi cha mguu) na Tomas Rosicky (kiazi cha mguu).

No comments:

Post a Comment