STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, January 3, 2014

Mata aonyeshwa mlango wa kutoka darajani

Mourinho akiwa na Mata
 KOCHA Jose Mourinho amemwambia Juan Mata anaweza 'kuchapa mwendo' (kuondoka) Chelsea baada ya kukasirika alipofanyiwa 'sabu' dakika ya 53 katika mechi ya kwanza ya mwaka mpya dhidi Southampton kwenye Uwanja wa St Mary's.
Mata alimpuuza Mourinho wakati alipokuwa akitoka uwanjani na kisha kukataa kugonga siti za wachezaji wa akiba.
Katika mchezo huo alitolewa na nafasi yake kuchukuliwa na Oscar, ambaye alionyeshwa kadi ya njano kutokana na 'kupiga mbizi' (kujirusha), na baada ya hapo kufunga bao wakati Chelsea ikishinda 3-0.
Mata amewahi kutwa tuzo ya mchezaji bora wa klabu katika misimu miwili iliyopita na alitajwa katika kikosi cha wachezaji wakulipwa cha msimu wa 2012/13.
Lakini sasa Mourinho amesema hawezi kumzuia Mhispania huyo kuondoka kama atataka kuchapa mwendo Stamford Bridge.
Mourinho, aliweka wazi kuhusu mchezaji huyo, kwa kusema: "Sitaki aondoke, hayo ndiyo maoni yangu na hilo ndilo ninalolitaka - lakini mlango wangu upo wazi.
"Mlango wa klabu upo wazi pia, hivyo kama mchezaji anataka kuzungumza na sisi tupo pale tunawasubiri. Lakini kama utaniluliza endapo ninata kumuuza, sihitaji pia.
"Sikuona alivyofanya, kutibuka kwake ni kwa sababu ya matokeo- tunahitaji kushinda.
"Kama hatukushinda mchezo huu, tofauti ya pointi kutoka timu inayoongoza ingekuwa kubwa. Mwishoni mwa mchezo kila mmoja akiwamo yeye walisherehekea ushindi."

No comments:

Post a Comment