STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, January 3, 2014

Yanga wajipange kwa Ashanti Utd, yapigwa na Tusker lakini....!

IKIWA na uchovu wa safari, Ashanti United iliyochukua nafasi ya Yanga kwenye michuano ya Kombe la Mapinduzi usiku wa jana ilianza vibaya kwa kulazwa bao 1-0 na Tusker ya Kenya, lakini ikionyesha kuimarika zaidi.
Ashanti inayonolewa kwa sasa na kocha Abdallah Kibadeni 'King' ilitua jana asubuhi visiwani humo na kushuka dimba la Amaan usiku na kuionyesha kazi Tusker kabla ya kukubali bao 1-0 lililofungwa dakika ya 24 na Joshua Oyoo.
Kwa muziki iliyouonyesha Ashanti, ni wazi Yanga itakuwa na kazi kubwa katika mechi ya fungua dimba ya duru la pili la Ligi Kuu Tanzania Bara inayoanza Januari 25.
Katika mechi ya kwanza baina ya timu hizo, Yanga iliisasambua Ashanti kwa mabao 5-1.
Michuano hiyo itaendelea tena jioni ya leo kwa michezo kadhaa ikiwemo la 'mnyama' Simba iliyoitafuna Leopards wa Kenya itashuka dimbani usiku kuwakabili watoza ushuru wa Uganda, URA.

No comments:

Post a Comment