STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, January 21, 2014

Balotelli amkaribisha Seedorf kwa ushindi Milan

Super Mario Bal;otelli

KOCHA mpya wa AC Milan Clarence Seedorf ameanza vyema kazi ytake ya kuiinoa timu hiyo aliyowahi kutamba nayo kwa ushindi wa bao 1-0,  shukrani zikimwendea Mario Balotelli aliyefunga kwa mkwaju wa penalti  kwenye mechi ya Serie A dhidi ya Verona juzi.
Mshambuliaji huyo alizamisha penalti hiyo kimiani katika dakika ya 82 baada ya Alejandro Gonzalez kumchezea madhambi Kaka ndani ya eneo la hatari.
Licha ya ushindi huo, mabingwa hao mara 18 wa Serie A, bado wanashika nafasi ya 11 katika ligi hiyo ambayo walikuwa wakiishika wiki iliyopita wakati Seedorf aliporithi mikoba ya Massimiliano Allegri aliyetimuliwa kutokana na matokeo mabaya.

No comments:

Post a Comment