STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, February 25, 2014

Ajali tena! Watu watano wafa Kilimanjaro, wanne taaban


PIcha hii haihusiki na habari hii, ila ni kati ya ajali ambazo zimekuwa zikichukua roiho za watanzania wenzetu kila uchao
AJALI za barabarani zimeendelea kuteketeza roho za watanzania baada ya watu watano kufariki katika ajali iliyohusisha magari mawili katika eneo la Boma Ng'ombe wilayani Hai mkoani Kilimanjaro.
Kwa mujibu wa taarifa zilizothibitishwa na jeshi la Polisi mkoani Kilimanjaro, watu hao walifariki jana jioni katika njia ya mzunguko ya uwanja wa ndege wa kimataifa ya KIA ikihusisha magari mawili yaliyogongana ubavuni ambapo watu wengine wanne walijeruhiwa.
Inadaiwa mwendo kasi ya magari hayo ndiyo yaliyosababisha vifo vya watu hao watano wakiwamo wanaume watatu na wanawake wawili ambao miili yao iliharibika.
Abiria wanne walionusurika kufa wapo katika hali mbaya na wamelazwa katika hospitali ya mkoa ya Maweni kwa ajili ya matibabu.

No comments:

Post a Comment